Suala la kumtambua mwanamke kuwa hana akili lina historia ndefu katika maandiko ya kifalsafa. Aristotle, wanafikra wa karne za kati na wanafalsafa wapya wa kiliberali wakiwemo Hume, Rousseau, Kant na Hegel wote walikuwa na shaka kuhusu suala kuwa mwanamke ana akili. Kwa msingi huo mafeministi wa kiliberali walitilia mkazo mitazamo yao ya kiliberali na kutetea wanawake katika suala la kutambua haki za kisiasa za watu kwa mujibu wa kiwango chao cha akili wakisema kuwa kubakia nyuma wanawake katika uwanja huo wa kisiasa ukilinganisha na wanaume, ni matokeo ya kunyimwa haki ya kupata suhula na fursa sawa na za wanaume. Dukuduku kubwa zaidi la mafeminsiti wa kiliberali lilikuwa haki zao za kisiasa na kisheria. Hivyo mapambano yao ya karne ya 19 hususan katika wimbi la kwanza la ufeministi yalifanyika kwa shabaha ya kurejesha haki za kumiliki wanawake walioolewa. Mafeministi wa kiliberali walitilia mkazo ubinadamu wa mwanamke na kutaka apewe nafasi sawa na ya mwanaume. Kwa msingi huo walitaka kuwepo usawa baina ya wanawake na wanaume katika fursa za kazi na kutaja kufanya kazi za nyumbani kuwa ni dhulma kwa mwanamke. Vilevile nafasi ya mama ni miongoni mwa mambo yaliyozusha mjadala mkubwa zaidi kati ya mitazamo ya mafeministi wa kiliberali ambao walitambua suala la kutoa mimba kuwa ni miongoni mwa haki za kimsingi za mwanamke (Wamitila, 2003).
Katika historia harakati za kudai haki za wanawake
zilianza katika Ulaya wakati haki za binadamu zilipoanza kutangazwa, ambazo awali
zilijadiliwa kwa wanaume pekee. Harakati ya kuwapa wanawake haki za kupiga kura
kwenye uchaguzi wa kisiasa ilikuwa kampeni ya
awali kuanzia karne ya
19.
Uhakiki
wa kifeministi ulishika kasi miaka ya 1960 na kuendelea kukua na kuishia kuwa
muhimu katika miaka ya hivi karibuni. Zipo kazi kadhaa zilizoandikwa kabla na
kuhimulika suala hili kwa namna moja ama nyingine. Kazi kuu mbili za “A Room of One’s Own” ya Virginia Woolf na “A virdiction of the Right of women “ya Mery Wollsto Necraft.
Zimechangia sana katika kutilia mkazo nadharia ya Ufeministi.
Williady
(2015) anasema kwamba nadharia hii inahistoria ndefu duniani, akimaanisha ni
moja ya nadharia zilizopata kutokea miongo mingi iliyopita. chanzo cha kuibuka
kwa nadharia hii ni vuguvugu la kutaka kufuta kabisa uonevu wa mwanaume kwa
mwanamke. Nadharia hii inadai kuwa chimbuko la uonevu na ukandamizaji
unaofanywa na wanaume kwa wanawake ni uroho wa mwanaume katika kumtawala
mwanamke. Kwa ufupi, ajaenda kuu ya ufeministi na mafeministi ni kumaliza
kabisa utawala wa mwanaume kwa mwanamke.
Mmoja
kati ya wadau waliochangia sana kuendelea kwa nadharia hii kwa kasi ni Adrew
Dworkin mwaka 1976 akiwa katika mji mkuu wa Uingereza; London, alitoa
mapendekezo makali katika kukomesha utawala wa mwanaume kwa mwanamke, Dworkin
anasema: Ili kufanikisha, tunahitaji kubomoa kabisa muundo wa mihimili ya
utamaduni wa jamii kama vile sanaa, kanisa, sheria, kaya zinazodhibitiwa na
baba, jamii na taswira zote za asasi, mila, desturi ambazo zinamwona
mwanamke kuwa mtu ovyo.
Hata
hivyo, kazi iliyoishia kuwa na mchango mkubwa katika kuuweka msingi wa uhakiki
wa ufeministi ni kazi maarufu ya mwandishi wa Kifaransa, Simone de Beauvoir
iitwayo, “The Second sex,” ya mwaka
1952. Katika kitabu hiki, mwandishi huyu anachukuwa mkabala wa kiharakati kwa
kushambulia na kukosoa baadhi ya asasi zinazochangia katika kumdhalilisha au
kumdunisha mwanamke. Asasi kuu anazozishambulia ni ndoa, dini na utamaduni.
Hata hivyo, nadharia ya ufeministi ilichimbuka huko Marekani katika harakati za
kukomesha biashara ya utumwa mwaka 1830 ambapo wanawake walianzisha harakati za
kupigania haki za mwanamke.
Malenya
(2012) anaeleza kuwa dhana ya ufeministi ilianza kujitokezaa kwa mara ya kwanza
baada ya Simone De Beauvoi aliyezaliwa huko Ufaransa akiwa ni mtoto wa kike na
wa kipekee katika familia yao na ambaye alionekana kama muhamasishaji wa kwanza
juu ya Ufeministi. Hii ilitokana na uwezo mwingi aliokuwa nao katika kufikiri,
hekima na bidii katika kazi vilivyosababisha kusifiwa daima na baba yake. Hali
hii ilianza kuibua mtazamo hasi dhidi ya wanawake baada ya baba yake kudai
kuwa, uwezo wa akili alionao unafanana na wake na wala sio kama wa mama yake.
Hali hii ilimfanya Simone De Beauvoi kujenga dhana ya unyanyasaji wa wanawake
na hata kumfanya asifikilie kuolewa bali ajikite na harakati za ukombozi kwa
wanawake. Kupitia harakati zake aliamsha hisia na hari kwa wanawake kutaka
kujikomboa. Baadhi ya nyanja zilizoonekana kumkandamiza mwanamke ni pamoja na
asasi za kijamii kama vile dini, tamaduni na uandishi mbalimbali wa kazi za
fasihi.
Malengo ya Nadharia ya Ufeministi
Wamitila
(2006:160-161) na Ntarangwi (2004:52-56) wamebainisha malengo mbalimbali ya
ufeministi. Ni kweli kwamba kuna baadhi ya malengo ya ufeministi yanakinzana na
maisha halisi ya mwanamke wa Kiafrika lakini baadhi ya malengo hayo yanasawiri
maisha halisi ya mwanamke wa kiafrika.
Nadharia ya ufeministi ina lengo la kuondoa
unyanyasaji wa kijinsia hasa kwa mwanamke. Hivyo basi, malengo ya ufeministi
yalijikita katika kumnasua mwanamke kutoka katika pingu za kisiasa, kiuchumi,
kiutamaduni na kijamii. Malengo haya ndiyo yanayoleta ukinzani wa maisha halisi
ya mwanamke wa Kiafrika. Hali hii imeleta mabadiliko katika maisha ya wanawake
wa kiafrika, kama vile kutaka haki ya elimu, kumiliki mali, kurithi mali,
kutaka nafasi za uongozi, pia kuwa na maamuzi ya kifamilia au kiukoo, katika
kupingana na pingu za maisha.
Dhana ya Ufeministi
Ufeministi (kutoka mzizi wa Kilatini ‘femina,’ yaani wa
‘kike’; au mwanamke. Kwa lugha ya kifaransa féminisme linamaanisha harakati ya ukombozi wa wanawake) ni jina linalojumlisha aina
nyingi za misimamo, itikadi na matapo tofautitofauti yanayochangia lengo kuu la kutetea haki za wanawake dhidi
ya ubaguzi
wa jinsia uliotawala dunia kwa
muda mrefu sana upande wa siasa, uchumi, utamaduni, dini na jamii kwa
jumla (Luvenduski & Randall, 1993).
Nadharia
ya Ufeministi imefasiliwa na wataalamu mbalimbali kama vile: Wamitila
(2003:253) anayesema kuwa hii ni nadharia ambayo imewekewa msingi na msukumo
mkubwa pamoja na nia ya kupigania ukombozi wa mwanamke kutokana na pingu za
kiutamaduni, kidini, kijamii, kisiasa na kiuchumi. Aidha, anaongeza kuwa
ufeministi ni nadharia ambayo inasaili na kudadisi itikadi ya kiume ambayo
imekuwepo katika jamii kwa kipindi kirefu. Kudadisi pia fasiri za kiume za
fasihi pamoja na mikabala ya kiubabedume.
Ntarangwi
(2004:45) anadai kuwa Ufeministi ni nadharia ambayo inajaribu kukiuka mitazamo
ya kiume ambayo yaelekea inatumiwa sana katika jamii. Anaendelea kusema kuwa
nadharia ya ufeministi imetokana na mkondo na harakati za kutetea haki za
wanawake ulimwenguni na imejikita katika imani ya usawa wa kijinsia, kijamii,
kisiasa na kiuchumi.
Williady
(2015) anasema kwamba ufeministi ni ninadharia iliyojaribu kuvunja mwiko wa
mfumo dume hapa dunia kwa kuanzisha mapambano ya usawa wa kijinsia, bilashaka
majaribio haya bado hayajafanikiwa. Anaongeza kwamba hayajafanikiwa kwa sababu
jamii inachukua muda kubadilika hivyo matarajio ya wanawake yatafikiwa tu kwa kuwa
hawakata tamaa.
Waandishi
wengine wanaendelea kuufafanua ufeministi kama istilahi inayotumiwa kueleza
nadharia ambayo imewekewa misingi na msukumo mkubwa pamoja na nia ya kupigania
ukombozi wa wanawake kutokana na pingu za kiutamaduni na kidini zilizomfunga
kwa muda Mrefu (Malenya, 2012).
Irib
(2014) anaongeza kuwa ufeministi ni harakati za ukombozi zilizoanzishwa na
wanawake ili kupinga mfumo dume ambao unawakandamiza wanawake katika nyanja
mbalimbali. Anaendelea kuunga mkono tafsiri ya Wamitilia kwamba, ufeministi ni
nadharia inayopinga asasi zote za kijamii zinazochangia katika kudhulumiwa kwa
mwanamke katika Nyanja mbalimbali.
Kwa
jumla, mwandishi anaiona nadharia ya ufeministi kama nadharia iliyojikita
katika kupinga ukandamizaji wa mwanamke unaofanywa na mwanaume katika jamii
hususan katika nyanja za kisiasa, kiuchumi, na kiutamaduni. Hivyo
basi, ufeministi ni harakati zinazofanywa na wanawake kujikomboa katika Nyanja
mbalimbali za: kifikra, kiuchumi, kisiasa, kijamii na kiutamaduni kutoka katika
mifumo ya ukandamizwaji.
Aina za Ufeministi na
Mikondo yake
Mgawanyiko umeanza kujitokeza kati
ya wale wanaotaka wanawake wafanane kabisa na wanaume na wale wanaoona umuhimu
wa kutunza upekee wa mwanamke katika uhusiano wa kukamilishana na mwanamume.
Kwa mfano: wengine husema wanaume na wanawake wanapaswa kutendewa sawa katika
mambo yote. Wanadhani hoja ya jadi kuwa wanawake wana kazi ya
kutunza nyumba na kuangalia watoto si sawa: wanawake na wanaume wanapaswa
kushiriki katika shughuli zote sawasawa. Wengine hukubali kwamba kuna tofauti
muhimu kati ya jinsia lakini tofauti hizo zisiruhusiwe kuwapa wanaume kipaumbele. Kama wanawake
wanapendelea kukaa nyumbani na kuangalia watoto ni sawa, lakini wasilazimishwe
kufanya hivyo, nao wanapaswa kupata namna ya malipo kwa kazi hiyo ama sehemu ya mapato ya familia au pia haki za malipo
ya pensheni kutoka serikali kwa
wakati wa uzee kwa ajili ya miaka waliyoitumia
kwa kazi ya nyumbani. Wengine
husema jamii imepokea utaratibu wake kutokana na mapenzi ya wanaume, hivyo ni
lazima kuwa na aina ya mapinduzi katika jamii. Na kuna wafuasi wa ufeministi
wanaoamini ya kwamba hakuna tofauti za maana kati ya jinsia lakini wengine
hufundisha kuwa wanawake ni tofauti kabisa na wanaume, na ni muhimu watoe
mchango wao wa pekee (Gabriel, 2010).
Malenya
(2012) anaibuka na kuugawa Ufeministi katika makundi mbalimbali yakiwemo ya
kiuharakati, kiutamaduni, kiuyakinifu na kadharika.
Ufeministi wa Kiharakati
Ufeministi
wa Kiharakati; huu ni ukombozi unaotambua kuwa mwanamke ananyanyaswa na
kukandamizwa na mwanaume hivyo kuona umuhimu wa kuwaelimisha wanawake kukataa unyanyaswaji
na ukandamizwaji dhidi yao. Aina hii inamwona mwanamme kama mkandamizaji wa
kwanza wa uhuru na haki za mwanamke. Hivyo basi, mwanamke anahamasishwa kuanza
harakati za ukombozi dhidi ya minyororo.
Ufeministi wa Kiutamaduni
Ufeministi
wa kiutamaduni; hii ni aina ya ufeministi ambayo inautizama utamaduni kama
nyenzo kubwa katika kumdhalilisha na kumfanya mwanamke aamini kuwa anapaswa
kuwa na hali aliyonayo mfano; kukandamizwa, kudhalilishwa na kukosa uhuru wa
kutoa maoni. Ufeministi unaotoa wito kwa kila mwanamke kuona umuhimu na wajibu
wa kushiriki katika ukombozi wa mwanamke. Tamaduni mbalimbali hasa za kiafrika
zimekuwa zikimgandamiza mwanamke katika mambo mbalimbali kwa mfano; wanawake
katika jamii ya Wahaya (kabila linalopatikana Bukoba mkoani Kagera)
hawakuruhisiwa kula nyama ya kuku au kula senene.
Ufeministi Huru
Hutetea
usawa kati ya wanawake na wanaume katika ngazi zote za maisha. Mkondo huu
hushikilia kwamba maadamu wanadamu wote ni sawa, wote wake kwa waume wanapaswa
kuwa huru katika kutekeleza malengo na majukumu yao ya kila siku.
Ufeministi wa Kiuyakinifu
Ufeministi
wa Kiuyakinifu; ni aina ya ufeministi ambao unamkomboa mwanamke katika misingi
ya kijinsia hususani katika utekelezajii wa majukumu mbalimbali ya kijamii
ikimaanisha kuwa mwanamke huchukuliwa kama mtu asiyeweza kusimamia na kufanya
baadhi ya majukumu au kazi kama ilivyo kwa mwanaume. Kwa mfano utabibu, ualimu,
uadhili, uongozi, ujenzi pamoja na upendeleo katika uelimishaji wa watoto wa
kike ambapo wavulana hupewa kipaumbele zaidi.
Ufeministi wa Kidhahania
Ufeministi
wa Kidhahania; ni aina ya ufeministi ambao unamwonesha mwanamke kama kiumbe
huru mwenye uwezo wa kuteua, kujilinda na kujitazama atakavyo mwenyewe.
Aidha,
mwanamke anaona kuwa hakuna haja ya mawazo yake kuamuliwa na mwanaume au mtu
yeyote katika jamii. Kutokana na dhana hii, jamii imeanza kuwapata wanawake
wanajeshi, wazalishaji mali, walimu na matabibu.
Ufeministi wa Kimaksi
Ufeministi wa kimaksi pia ni miongoni mwa
mielekeo ya ufeministi. Kundi hili liliamini kuwa chanzo dhulma dhidi ya
mwanamke ni kukandamizwa kwao kiuchumi, kijamii na kisheria akilinganishwa na
mwanaume na linasema dhulma hiyo itakomeshwa kwa kubadilishwa haki za kijamii
na kiuchumi. Mafeministi wa kimaksi wanamtambua mwanawake kuwa ni mithili ya
vibarua katika makucha ya wanyonyaji na wanatumikia maslahi ya mfumo wa
ubepari. Wanaamini kuwa wawekezaji wanatumia nguvu rahisi ya wanawake na watoto
kwa shabaha ya kupunguza gharama za uzalishaji. Kwa msingi huo mafeministi wa
kimaksi wanasisitiza juu ya udharura wa kufutwa mfumo wa kibepari na kukomeshwa
dhulma dhidi ya wanawake. Kundi hili la mafeministi pia linashabihisha kazi ya
kuzaa na kujifungua mwanamke na mwenendo wa wananyama na si kitendo cha
kibinadamu.
Karl Marx na Engels wakinukuliwa na Malenya
(2012), walikuwa wakiamini kwamba familia ndiyo taasisi ya kwanza ya kijamii
ambako hakuna usawa katika kugawa kazi baina ya mwanamke na mwanaume na kwamba
mfumo huo wa familia unapaswa kuangamizwa na badala yake kuanzishwe taasisi za
ushirika au ujima ili kazi za nyumbani, kulea watoto na kadhalika zifanywe na jinsia
mbili kwa usawa. Fikra hizi za kimaksi zilivuruga mipaka ya kifamilia na
kupuuza uhakika wa kijamii. Vilevile mafeministi wa kimaksi waliamini kuwa,
dhulma dhidi ya wanawake zinatokana na mfumo dume na ubepari, wakati hakuna
mfungamano wa aina yoyote baina ya viwili hivyo.
Ufeministi wa Kisoshalisti
Ufeministi wa kisoshalisti ni katika milengo ya
harakati ya ufeministi. Mlengo huu pia unasema kuwa uhusiano baina ya wanawake
na wanaume unatokana na muundo wa kijamii na kiuchumi na mageuzi makubwa au
mapinduzi ya kijamii, na kwamba kuwepo haki sawa kati ya wanawake na wanaume
kumo katika usawa wa kijamii na kufutwa kabisa dhulma ya kijinsia na kitabaka.
Mafeministi wa kisoshalisti wanasema mfumo wa kugawa kazi kwa mujibu wa jinsia
ya mtu na kubana sehemu za kazi za wanawake ndani ya nyumba na kazi za mama
ulibuniwa kwa ajili ya kudhamini maslahi ya kiuchumi ya ubepari. Mafenisti hawa
wa kisoshalisti wanakubaliana na uchambuzi wa wenzao wa kimaksi kuhusu uhusiano
wa kitabaka wa ubepari, kwa msingi huo wanasisitiza kuwa ili kupatikana usawa
na kubadili hali ya sasa kuna ulazima kuwepo mapambano dhidi ya mfumo dume na
ubepari. Wanasema mapambano hayo yanapaswa kupanuliwa zaidi kuanzia maeneo ya
viwandani hadi kazi zote za umma na za binafsi ambako wanawake wanabaguliwa
(Gabriel, 2010). Moja ya matatizo makubwa ya mtazamo huu ni
kwamba unayafanya maisha ya mwanaume na mwanamke kuwa uwanja wa vita na
mpambano baina ya jinsia hizo mbili ilhali, kimaumbile, kila mmoja kati ya
wawili hao ana nakisi na mapungufu ambayo hayawezi kuondolewa isipokuwa kwa
ushirikiano na maelewano baina yao.
Ufeministi wa Kuchupa Mipaka (radical
feminism)
Mlengo mwingine wa ufeministi ni
ule wenye misimamo mikali ya kuchupa mipaka (radical feminism). Mafeministi
hawa wenye misimamo mikali wanadai kuwa, dhulma zinazofanyika kwa msingi wa
jinsia ndizo kubwa zaidi ya zote na kwamba zinatokana na mfumo dume
(Patriarchy). Wanasisitiza kuwa wanaume au kwa ujumla mfumo dume ndiyo sababu
kuu ya dhulma zinazowasibu wanawake na kwamba sheria zisizo za kiadilifu
zinachangia pia katika mfumo kandamizi unaompa mwanaume mamlaka kamili kuanzia
katika familia hadi katika taasisi za kisiasa. Mafeministi hawa wenye misimamo
mikali wanasema wanaume wote ni wakatili na wadhalimu dhidi ya wanawake na
kwamba kunahitajika mapinduzi makubwa ya kuondoa hali hiyo na si kubadili
sheria za kisiasa na kijamii tu (Gabriel, 2015). Mafeministi hawa wanafikia kiwango cha kutoa wito wa
kuuawa na kufutwa kabisa wanaume! Misimamo ya kupindukia mipaka ya mafeninisti
hawa sambamba na mitazamo yao kama ile ya kupuuza tofauti za kimaumbile kati ya
mwanamke na mwanaume, kupuuzwa haki za wanawake kama wale wenye asili ya Afrika
au weusi na kumtwisha mwanamke majukumu mazito ya kimaisha, ilikabiliwa na
malalamiko na upinzani mkubwa hata ndani ya jamii ya wanawake. Kwa msingi huo
katika wimbi la tatu la ufeministi kulitolewa wito wa kutazamwa upya na
kufanyika mabadiliko katika mitazamo ya ufeministi.
Misingi ya Nadharia ya Ufeministi
Mchango mkubwa katika
kuweka msingi wa uhakiki wa ufeministi ni kazi maarufu ya mwandishi wa
Kifaransa, Simone de Beauvoir iitwayo, “The Second sex,” ya
mwaka 1952. Katika kitabu hiki, mwandishi huyu anachukuwa mkabala wa kiharakati
kwa kushambulia na kukosoa baadhi ya asasi zinazochangia katika kumdhalilisha
au kumdunisha mwanamke. Asasi kuu anazozishambulia ni ndoa, dini na utamaduni. Miongoni mwa misingi ya kifikra ya ufeministi ni pamoja na:
·
kupinga na kutupilia
mbali mafundisho ya dini. Mafemenisti wanayaona mafundisho ya dini kuwa
yanachangia katika kuimarisha utamaduni wa mfumo dume, kwa msingi huo wanaamini
na kufuata thamani za kimaada na kupinga thamani za kidini. Wanasema thamani na
mafundisho ya dini ndiyo kizuizi kikuu katika njia ya kufikiwa malengo yao
kwani wanaamini kuwa dini za Mwenyezi Mungu zinathamini na kutukuza sana
familia na nafasi ya mama, na ili kulinda nafasi hiyo zinamzuia mwanamke
kushiriki katika baadhi ya mambo ya kisiasa, kijamii, kiuchumi na kadhalika.
Vilevile wanasema dini zinashajiisha na kuhamasisha uzazi na kuzaa, na zinakataza
kuavya mimba na kuwalazimisha watu kuzilinda na kulitambua suala hilo kuwa ni
sawa na kulinda nafsi ya mwanadamu mzima. Hivyo basi kuna haja ya kufanyika
jitihada za kujiweka mbali na thamani na mafundisho ya dini!
·
Nadharia hii inatumika
fasihi kama jukwaa la kueleza kwa uyakinifu hali aliyonayo mwanamke ili
kumsaidia kumwzwsha mtu yeyote kuielewa hali hiyo na kisha kumsaidia mwanamke.
Fsihi imekuwa ikitumiwa na Waandishi mbalimbali katika kazi zao kumwelezea
mwanamke na adha anayoipata katika jamii yake.
·
Nadharia hii inanuia
kuwasawazisha wanadamu kwa upande wa utamaduni na uana. Inapigania jamii mpya
yenye msingi katika amali za kibinadamu. Baadhi ya amali hizo ni zile za kike
na za kijadi na ambazo zinadharauliwa katika jamii ya sasa.
·
Mitazamo huu Vilevile
unajaribu kuhamasisha utungaji wa kazi za sanaa zenye wahusika wa kike
wanaoweza kuhigwa (kuwa mfano), wanawake ambao hawategemei wanaume ili
wajitambulishe. Kazi hii yaweza kufanywa na wanaume ili kuonyesha ya kwamba
wanakubaliana na uwezo wa mwanamke kusimama peke yake na kujitambilisha katika
Nyanja zote za kisiasa, kiuchumi na kijamii.
·
Inaendeleza na kukuza
hisia za umoja wa wanawake kama Kundi linalodhulumiwa. Hii itasaidia kuzindua
na kuleta mwamko kwa upande wanawake jinsi wanavyojiona na uhusiano wao na watu
wengine.
·
Nadharia hii
inadhamilia kuvumbua na kuziweka wazi kazi za kifasihi zilizotungwa na wanawake
na ambazo zimepuuzwa kwa sababu ya utamaduni unaopendelea wanaume. Kisha kuwahamasisha
wanawake kujitokeza kwa wingi katika utunzi wa kazi za kifasihi ili kuptia humo
waweze kupaza sauti zao.
Wafeministi wanaamini kuwa mtazamo
jumla wa jamii nyingi unawadunisha wanawake na kuwafanya watu wa daraja la
pili. Kwa msingi huo wanasisitiza juu ya kubadilishwa mtazamo wa jamii kuhusu wanawake
na kufutwa ubaguzi unaolenga jamii hiyo. Hapa inatupasa kusema kuwa, kila mtu
mwenye insafu anajua kwamba, mijadala inayohusiana na haki za wanawake na
mafeministi na wito wa kufanyika mabadiliko katika mtazamo unaowaona wanawake
kuwa ni wanadamu wa daraja la pili katika nchi za Magharibi na vilevile juhudi
za mafeministi za kupigania haki zao za kisiasa, kijamii na kichumi vimepelekea
kupatikana baadhi ya mafanikio kwa maslahi ya wanawake hususan katika nchi za
Magharibi. Hata hivyo suala la kupigania haki za wanawake na kupambana na
ubaguzi halipasi kuwa kisingizio cha kutokomeza na kuua maana ya maisha,
kumdunisha mwanaume katika jamii na kulazimisha haki na majukumu sawa na
yanazofanana licha ya tofauti za kimaumbile baina ya jinsia mbili za wanadamu
(Irib, 2014).
Uislamu
sio pekee wenye itikadi ya kuwatukuza wanaume bali watu mbalimbali toka katika
dini za Uyahudi (agano la kale), Ukristo na Uislamu pia katika Quran. Dini zote
zinawatukuza wanaume kwa sababu zimeanzishwa kutokana na misingi ya jamii zenye
kutukuza wanaume. Mtafiti anasema kuwa hata hijabu kwa wanawake sio tu kwa
waislamu pekee, ni kwa utamaduni wa kale uliorithiwa na wenye kufanana na dini
ya kisita (utawa) (Nyangasa, 2016).
Katika
andiko la the Global and mail octoba 4, 1994, mwanafunzi msichana wa Kiislam
avaae kitambaa cha kufunika kichwa alinyimwa haki yake ya kupata elimu nchini
Ufaransa. Lakini jambo la kujiuliza ni kwamba; je dini za Uislam, Ukristo na Uyahudi
zinafanana juu ya wanawake? Au dini za Ki-risto huwatendea vyema wanawake
kuliko Waislam?. Nafasi ya mwanamke katika dini hizi tatu inatokana na ushahidi
wa maandiko ya vitabu vitakatifu vya Quran, Hadithi za mtume (S.A.W), Biblia,
Talmudi (Kitabu cha Wayahudi) (Yangasa, 2016).
Kosa la Hawa (Eva)
Dini
hizi tatu zinakubaliana ya kwamba wanawake na wanaume wote wameumbwa na Mungu.
Lakini tofauti zinaanzia pale tu mwanaume alipoumbwa wa kwanza na mwanamke
kutokea ubavuni mwa mwanaume (Mwanzo, 2:4-3:24). Lakini Mungu aliwakataza wote
wawili wasile matunda ya mti uliokatazwa katika bustani walimoishi. Nyoka
alimshawisi Hawa ale tunda la mti huo na kisha Hawa akamshawishi Adam ale
pamoja naye. Hivyo, lawama zilimwendea Hawa kwa mfano “huyu mwanamke uliyenipa
awe pamoja name ndiye aliyenipa matunda ya mti huo nikala (Mwanzo, 3:12) na
katika (Mwanzo 3:16) “…akamwambia mwanamke, hakika nitakuzidishia uchungu wako,
na kuzaa kwako; kwa utungu utazaa Watoto; na tama yako itakuwa kwa mumeo, naye
atakutawala.
Katika
Quran takatifu uumbaji unazungumziwa katika sehemu nyingi mfano “kisha Mungu
akasema akimwambia nabii Adam..Nawe Adam! Kaa peponi pamoja na meko, na kuleni
mnapopenda, lakini msiukalibie mti huu msije kuwa miongoni mwa waliodhurumu
nafsi zao. …Mola wenu hakuwakataza mti huu (kwa sababu hii) msije mkawa Malaika
au kuwa miongoni mwa wakaao milele (Quran 7:19-23). Mitazamo yakinifu toka vitabu
hivi viwili inatoa lawama kwa watu wote wawili (Adam na Hawa). Lakini katika
Quran hakuna kipengele hata kimoja kinacho eleza kuwa Hawa ndiye alimshawishi
Adam kula tunda au kwamba Hawa ndiye alikula tunda wa kwanza au Hawa ndiye
alimpelekea Adam. Kwa mantiki hii Quran haimwiti Hawa mshawishi wa Adam kula
tunda na Hawa si mlaghai wa mdanganyifu.
Urithi wa Hawa
Taswira
ya kuwa Hawa ni mshawishi iliyo ndani ya Biblia imeleta matokeo ya athari mbaya
kwa kiasi kikubwa kwa wanawake katika mafundisho ya Uyahudi-Ukristo. Wanawake
wote waliaminiwa kuwa wamerithi kutoka kwa mama yao Hawa wa Kibiblia mambo
mawili: zambi zake na hila zake. Kwa hiyo, wanawake wote wakawa hawaaminiwi,
madhaifu, uadlifu, na waovu. Kupatwa na hedhi, mimba, na kuzaa; vitu hivi
vilizingatiwa kuwa ni adhabu ya uadilifu kwa dhambi ya milele ya kulaaniwa kwa
jinsi ya kike.
Ili
tufahamu vizuri ni naman gani mkanganyiko mbaya juu ya Hawa wa Ki-biblia
ulivyokuwa kwa vijukuu vyake vya kike vyote tunalazimika kutazama maandiko ya
baadhi ya Wayahudi na Wakristo muhimu sana wa kila zama. Tazama Agano la Kale
na tuone dondoo kutoka katika kile kiitwacho Maandiko ya Busara ambayo kwayo
tunakuta: “Naona uchungu sana kuliko uchungu wa kifo mwanamke ambaye ni
ghiliba, ambaye moyo wake ni mtego na mikono yake ni minyororo. Mwanamume
anayempendeza Mungu atamuepuka mwanamke huyo, lakini muovu atatekwa na mwanamke
huyo… Wakati nilipokuwa naendelea kutafuta bila kupata, nilipata mwanamume
mmoja wa kuaminika miongoni mwa maelfu, lakini sijapata hata mwanamke mmoja wa
kuaminika miongoni mwa wanawake wote’’. (Ecclesiastes 7:26-28). Katika sehemu
nyingine ya maandiko ya Kiyahudi ambayo yanapatikana katika Biblia ya
Kikatoliki tunasoma: “Hakuna uovu unaotokea sehemu yeyote unaokaribiana na uovu
wa mwanamke…. Dhambi huanza kwa mwanamke na tunamshukuru mwanamke kwa kuwa sote
lazima tufe’’; (Ecclesiasticus 25:19-24).
Wataalamu
wa dini ya Kiyahudi wameorodhesha laana tisa zinazowatesa wanawake ikiwa ni
matokeo ya Kuporomoka: “Yeye ametoa laana tisa na kifo kwa mwanamke: Mzigo wa
damu ya hedhi na damu ya bikra; mzigo wa kubeba mimba; mzigo wa kuzaa; mzigo wa
kulea watoto; kichwa chake kinafunikwa kama vile mtu yupo katika maombolezo;
mwanamke anatoboa masikio yake kama vile mtumwa wa kudumu au mjakazi ambaye
anamtumikia bwana wake; mwanamke asiaminiwe kuwa ni shahidi; na baada ya yote
hayo… kifo.” Wayahudi wakiume wa
Kiorthodoksi katika sala zao za kila siku asubuhi wanakariri “Baraka ni za
Mungu mfalme wa ulimwengu wote kwa kuwa hajaniumba mwanamke”;
Wanawake, kwa upande mwingine, wanakariri “shukraniii ni za Mungu
kila asubuhi kwa kuniumba kulingana na Matakwa yake (Ecclesiasticus25:19-24).”
Sala
nyingine inayopatikana katika vitabu vingi vya sala za Kiyahudi ni: “Shukrani
ni za Mungu kwa kuwa hajaniumba nikiwa mtu wa mataifa (mtu ambaye si Myahudi).
Leonard and Swidler (1976:115) katika kazi yao iitwayo “Women in Judaism; the Status of Women in Formative Judaism” inasema: “Shukrani ni za Mungu kwa kuwa hajaniumba mwanamke. Shukrani ni za Mungu kwa kuwa hajaniumba mjinga.” Ushahidi huu unaendelea kuweka wazi jinsi Vitabu vitakatifu vya kikristo na kiyahudi vinavyo wabeza na kuwabagua wanawake.
Leonard and Swidler (1976:115) katika kazi yao iitwayo “Women in Judaism; the Status of Women in Formative Judaism” inasema: “Shukrani ni za Mungu kwa kuwa hajaniumba mwanamke. Shukrani ni za Mungu kwa kuwa hajaniumba mjinga.” Ushahidi huu unaendelea kuweka wazi jinsi Vitabu vitakatifu vya kikristo na kiyahudi vinavyo wabeza na kuwabagua wanawake.
Hawa wa Kibiblia amechukua sehemu kubwa katika Ukristo kuliko katika Uyahudi. Dhambi yake imekuwa ni tegemeo kwa imani yote ya Kikristo kwa sababu itikadi ya Kikristo juu ya sababu za kazi ya Yesu Kristo Duniani imejengwa kutokana na maasi ya Hawa wa Biblia kwa Mungu. Hawa alifanya dhambi kisha alimshawishi Adam afuate mkumbo wake. Kwa hiyo, Mungu aliwafukuza wote wawili watoke Peponi waende ardhini, ardhi ambayo imelaaniwa kwa ajili yao. Walirithisha dhambi yao, ambayo haikusamehewa na Mungu, kuwarithisha kizazi chao chote na kwa hiyo, binadamu wote wanazaliwa wakiwa na dhambi. Ili kuwatakasa wanadamu kutoka katika “dhambi zao za asili,” Mungu alilazimika kumtoa muhanga msalabani, Yesu, ambaye anazingatiwa kuwa ni mwana wa Mungu. Kwa hiyo, Hawa anabeba kosa lake, dhambi ya mumewe, dhambi ya asili ya binadamu wote, na kifo cha Mwana wa Mungu. Kwa maneno mengine, matendo ya mwanamke mmoja kwa nafsi yake yamesababisha kuangamia kwa binadamu.
Mt.
Tertullian pia alikuwa butu mno kuliko Mt. Paulo, alipokuwa akiongea na ‘watawa
wake awapendao sana kiimani, alisema: Je, kuna nini kwa mabinti zake? Hao nao
ni wakosaji kama yeye na wanalazimika kutendewa kama alivyotendewa yeye.
Sikiliza muono wa kuhuzunisha wa mtakatifu Paulo katika Agano Jipya: “Mwanamke
na ajifunze katika utulivu, akitii kwa kila namna. Simpi mwanamke ruhusa ya
kufundisha, wala kumtawala mwanamume, bali awe katika utulivu. Kwa maana Adamu
ndiye aliyeumbwa kwanza, na Hawa baadaye. Wala Adamu hakudanganywa, ila
mwanamke alidanganywa kabisa akaingia katika hali ya kukosa.” (1 Timotheo2:11-14).
Ruether
(1987:209) katika kazi yake ya For all
the sayings of the Prominent Saints, see Karen Armstrong, The Gospel According
to Woman anasema kwamba “Je, hivi hamjui kuwa nyinyi nyote ni akina Hawa?
Hukumu, (Maelezo) ya Mungu juu ya jinsia yenu yanaishi katika zama hizi: uovu
nao lazima uwe unaishi. Nyinyi ni mlango wa Shetani: Nyinyi ndio waondoaji
kizuizi cha mti ulioharamishwa: Nyinyi ndio wa mwanzo kuacha sheria takatifu:
Nyinyi ndio yule mwanamke aliyemshawishi mwanamume ambaye shetani alishindwa
kupata ujasiri wa kutosha kumvamia; niyinyi ndio mlioharibu kirahisi picha ya
Mungu. Kwa sababu ya dhambi zenu hata Mwana wa Mungu amelazimika afe.” Mt.
Augustine alikuwa ni mwaminifu kwa waliomtangulia, alimuandikia rafiki yake:
“Hakuna tofauti kwa mwanamke awe mke au mama, ataendelea kuwa ni Hawa tu ambaye
ni mshawishi kwa hiyo, lazima tujihadhari na mwanamke yeyote yule… Nimeshindwa
kupata faida ya mwanamke kwa mwanamume, ukitoa tendo la mwanamke kuweza kuzaa
watoto kadri mmewe atakavyo mzalisha.”
Baada ya karne kadhaa, Mt. Thomas Aquinas aliendelea kuamini kuwa wanawake ni wasaliti: “Kwa mintarafu ya tabia ya kimaumbile ya kila mmoja, mwanamke ni masaliti na ni mwanaharamu, kwa nguvu iliyo hai, kwa mbegu ya mwanamume inaelekea kutoa tunda lenye kufanana kikamilifu na jinsia ya kiume; huku tunda la mwanamke linakuja kutoka katika dosari ndani ya nguvu iliyohai au kutoka katika baadhi ya malighafi mbovu, au hata kutoka baadhi ya athari za nje.” Mwisho, mwanamageuzi mashuhuri Martin Luther hajaona faida yoyote kwa mwanamke ispokuwa kuleta watoto wengi duniani kwa kiasi kinachowezekana bila kujali athari mbaya zozote: “Kama watachoka au kufa, hakuna tatizo. Waache wafe kwa kuzaa, kwani hiyo ndio sababu ya kuwepo kwao.” Tena na tena wanawake wote ni wa kuadhiriwa kwa sababu ya taswira ya Hawa ambaye ni mlaghai, shukrani zende kwa fikra iliyopo katika kitabu cha Mwanzo. Kwa muhtasari, itikadi ya Kiyahudi-Kikristo juu ya Mwanamke imetiwa sumu kwa imani ya kuamini dhambi ya asili ya Hawa na watoto wake wa kike.
Baada ya karne kadhaa, Mt. Thomas Aquinas aliendelea kuamini kuwa wanawake ni wasaliti: “Kwa mintarafu ya tabia ya kimaumbile ya kila mmoja, mwanamke ni masaliti na ni mwanaharamu, kwa nguvu iliyo hai, kwa mbegu ya mwanamume inaelekea kutoa tunda lenye kufanana kikamilifu na jinsia ya kiume; huku tunda la mwanamke linakuja kutoka katika dosari ndani ya nguvu iliyohai au kutoka katika baadhi ya malighafi mbovu, au hata kutoka baadhi ya athari za nje.” Mwisho, mwanamageuzi mashuhuri Martin Luther hajaona faida yoyote kwa mwanamke ispokuwa kuleta watoto wengi duniani kwa kiasi kinachowezekana bila kujali athari mbaya zozote: “Kama watachoka au kufa, hakuna tatizo. Waache wafe kwa kuzaa, kwani hiyo ndio sababu ya kuwepo kwao.” Tena na tena wanawake wote ni wa kuadhiriwa kwa sababu ya taswira ya Hawa ambaye ni mlaghai, shukrani zende kwa fikra iliyopo katika kitabu cha Mwanzo. Kwa muhtasari, itikadi ya Kiyahudi-Kikristo juu ya Mwanamke imetiwa sumu kwa imani ya kuamini dhambi ya asili ya Hawa na watoto wake wa kike.
Katika
Quran maandiko yanasema: “Bila shaka wanaume wenye kufuata vizuri nguzo za
Uislamu, na wanawake wanaozifuata vizuri nguzo za Uislamu; na wanaume
wanaoamini vizuri nguzo za Imani, na wanawake wanaoamini vizuri nguzo za Imani;
na wanaume wanaotii, na wanawake wanaotii; na wanaume wasemao kweli, na
wanawake wasemao kweli; na wanaume wanaosubiri, na wanawake wanaosubiri; na
wanaume wanaonyenyekea na wanawake wanaonyenyekea; na wanaume wanaotoa Zaka na
sadaka na wanawake wanaotoa Zaka na sadaka, na wanaume wanaofunga; na wanawake
wanaofunga; na wanaume wanaojihifadhi tupu zao; na wanawake wanaojihifadhi; na
wanaume wanaomtaja Mungu kwa wingi; na wanawake wanaomtaja Mwenyezi Mungu;
amewaandalia msamaha na ujira mkubwa…” (Quran 33:35) “Na wanaoamini wanaume na
wanaoamini wanawake ni marafiki kwani huyaamrisha yaliyo mema na huyakataza
yaliyo mabaya na husimamisha sala na hutoa Zaka na humtii Mwenyezi Mungu na
Mtume wake… Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu na
Mwenye hikima. (Quran 9:71) “Mola wao Akawakubalia (maombi yao kwa kusema):
“Hakika Mimi sitapoteza juhudi (amali) ya mfanya juhudi miongoni mwenu, akiwa
mwanamume au mwanamke, (kwani nyinyi) ni nyinyi kwa nyinyi….” (Quran 3:195).
“Afanyaye ubaya hatalipwa ila sawa na huo uwovu wake na afanyaye mema, akiwa
mwanamume au mwanamke, naye ni Mwislamu, basi hao wataingia Peponi, waruzukiwe
humo bila hisabu.” (Quran 40:40)
Mabinti
Wanaotia Aibu
Kwa
hakika, Biblia inaeleza juu ya unyanyasaji wa jinsia ya kike kuanza punde tu
anapozaliwa mwanamke. Kwa mfano, Biblia inaeleza kuwa kipindi cha mama aliyezaa
kuwa si msafi kwa mujibu wa sheria za kidini ni mara mbili ya urefu wa kawaida
ikiwa mtoto atakuwa mwanamke kinyume na mwanamume. (Mambo ya Walawi 12:2-5).
Biblia ya Kikatoliki inaeleza kikamilifu kuwa: “Kuzaliwa kwa binti ni hasara”
(Ecclesiasticus 22:3). Kinyume cha maelezo haya yanayotia mshtuko na kupaza
roho, watoto wa kiume wanapokea sifa za kipee: “Mwenamume anayemuelimisha
mwanawe wa kiume atahusudiwa na maadui zake” (Ecclesiasticus 30:3).
Wanazuoni
wa Kiyahudi wameamrisha Wayahudi wa kiume wazaliane watoto wengi ili waendeleze
kabila la Kiyahudi. Wakati huo huo, hawafichi upendeleo wao wa wazi kwa watoto
wa kiume: “Ni uzuri kwa wale wote ambao watoto wao ni wa kiume lakini ni ubaya
kwa wale wote ambao watoto wao ni wanawake”, “Anapozaliwa mtoto wa kiume, watu
wote wanashangilia…. na anapozaliwa mtoto wa kike watu wote wanahuzunika” na
“wakati mtoto wa kiume anapokuja duniani, amani inakuja duniani…” Wakati mtoto
wa kike anapokuja duniani hakuna kitu kinachokuja.
Elimu kwa Wanawake
Moyo
wa Uyahudi ni Torati, ambayao ni sheria. Hata hivyo, kulingana na kitabu
Talmudi, (kitabu muhimu sana kwa Waislam), kinasema: “wanawake hawaruhusiwi
kujifunza Torati.” Baadhi ya wanazuoni wa Kiyahudi kwa ukali wametangaza kuwa
“ni bora kuyaacha maneno ya Torati yaunguzwe moto kuliko kusomwa na mwanamke”
na “Yeyote atakayemfundisha Torati binti yake amemfundisha uchafu.” “Mwenyezi
Mungu amekwishasikia usemi wa mwanamke yule anayejadiliana nawe sababu ya
mumewe, na anashtaki mbele ya Mwenyezi Mungu; na Mwenyezi Mungu anayasikia
majibizano yenu; hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia na Mwenye kuona.”
(Quran 58:1). Aidha Watoto wa jamii ya kiislamu wanapaswa kujifunza elimu
akhera na sio elimu dunia maana ufalme wa Alah (Mungu) si kwa mambo ya kidunia.
Mtazamo
wa Mt. Paulo katika Agano jipya anasema: “Wanawake na wanyamaze katika kanisa,
maana hawana ruhusa kunena; bali watii, kama vile inenavyo Torati nayo. Nao
wakitaka kujifunza neno lo lote, na wawaulize waume zao wenyewe nyumbani mwao;
maana ni aibu wanawake kunena katika kanisa” (Wakorintho wa Kwanza 14:34-35).
Vipi mwanamke ataweza kujifunza ikiwa haruhusiwi kuongea? Vipi mwanamke atakua
kiakili ikiwa amelazimishwa kuwa katika hali ya utiifu kikamilifu? Vipi
mwanamke ataweza kujipanua upeo wake wa kielimu ikiwa chanzo chake cha pekee
cha kupata elimu ni mumewe tu akiwa nyumbani?
Mama
mmoja aitwaye Khawlah akawa na wakati mgumu sana. Bibi huyo akaenda moja kwa
moja hadi kwa Mtume wa Uislamu ili kutetea kesi yake. Mtume (S.A.W) alikuwa na
rai ya kumtaka bibi huyo awe mtulivu kwa kuwa hakuna njia ya kutatua tatizo
hilo kwa wakati huo. Khawlah akaendelea kujadiliana na Mtume (S.A.W) akijaribu
kuokoa ndoa yake iliyotundikwa. Punde tu, Quran ikaingilia kati; na maombi ya
Khawlah yakakubaliwa. Hukumu takatifu ikakomesha tabia hiyo mbaya sana. Sura
moja kamilifu (sura ya 58) ya Quran inaitwa “Almujadilah” au “mwanamke ambaye
amefanya mjadala” iliitwa hivyo kwa ajili ya tukio hilo: Mwanamke katika
itikadi ya Quran anayo haki ya kupinga rai, hata kama ni rai ya Mtume wa Uislam
(S.A.W). Hakuna mwenye haki ya kumnyamazisha Mwanamke. Mwanamke hayupo chini ya
amri ya kumtaka mumemewe awe ndiye marejeo yake ya pekee katika masuala ya
kisheria na kidini.
Mwanamke Mwenye Hedhi
Sheria
na hukumu za Kiyahudi juu ya hedhi ya wanawake ni kali mno. Agano la kale
linamchukulia mwanamke yeyote mwenye hedhi kuwa si msafi na ni najisi. Zaidi ya
hayo unajisi wake “unaambukiza” wenginewe vile vile. Mtu yeyote au kitu
chochote atakachokigusa kitanajisika kwa siku nzima: “Mwanamke ye yote, kama
anatokwa na kitu, na kitu chake alichokuwa nacho mwilini mwake ni damu, ataketi
katika kutengwa kwake muda wa siku saba; na mtu ye yote atakayemgusa atakuwa
najisi hata jioni. Na kitu cho chote akilaliacho katika kutengwa kwake kitakuwa
najisi; na kila kitu ambacho akiketia kitakuwa najisi. Mtu ye yote
atakayekigusa kitanda chake huyo mwanamke atazifua nguo zake, na kuoga majini,
naye atakuwa najisi hata jioni. Mtu yeyote atakayekigusa cho chote ambacho huyo
mwanamke amekiketia atazifua nguo zake, na kuoga majini, naye atakuwa najisi
hata jioni. Kwamba, ni katika kitanda au cho chote alichokilalia huyo mwanamke
atakapokigusa kitu hicho atakuwa najisi kwa wakati huo na hata jioni (Law,
15:19-23). Kwa sababu ya maumbile yake ya kutia najisi; mwanamke mwenye hedhi
mara nyingine alipelekwa uhamishoni ili kuepusha uwezekano wowote wa kukutana
naye. Hupelekwa nyumba maalumu ziitwazo “nyumba ya wasio wasafi” kwa kipindi
chote cha hedhi yake. Zaidi ya hayo, mume wa mwanamke mwenye hedhi alizuiwa
kuingia sinagogini kama atachafuliwa na mkewe tena hata kwa mavumbi yaliyo
chini ya miguu yake.
Kasisi
yeyote ambaye mkewe, bintiye, au mamaye ni mwenye hedhi hakuruhusiwa kuhubiri
baraka sinagogini. Talmudi inamchukulia mwanake mwenye hedhi ni “mauti” hata
kama hakuna mafungamano ya kimwili: “Walimu zetu wa dini ya Kiyahudi
wametufunza… kama mwanamke mwenye hedhi atapita kati ya (wanaume) wawili, ikiwa
ni mwanzoni mwa hedhi yake, mwanamke huyo atamnyonga mmoja wao, na kama akiwa
mwishoni mwa hedhi yake, atasababisha ugomvi kati ya wanaume hao” (Bpes.111a.).
Haki
ya Kutoa Ushahidi
Kadhia
nyingine ambayo Quran na Biblia hazikubaliani ni kadhia ya mwanamke kutoa
ushahidi. Ni kweli kuwa Quran imewafunza waumini ambao wanashughulika na
mikataba ya kibiashara wawe na mashahidi wawili wa kiume au mwanamume mmoja na
wanawake wawili (Quran 2:282). Hata hivyo, ni kweli kwamba Quran katika matukio
mengine (baadhi) inakubali ushahidi wa mwanamke. Na kwa hakika ushahidi wa
mwanamke unaweza ukawa ni bora zaidi kuliko wa mwanamume katika baadhi ya mambo.
Kwa
upande mwingine, katika jamii za kale za Kiyahudi wanawake hawakuruhusiwa kutoa
ushahidi. Wanazuoni wa Kiyahudi waliwahesabu wanawake kuwa hawawezi kutoa
ushahidi. Jambo hilo ni miongoni mwa laana tisa zinazowatesa wanawake wote kwa
sababu ya “kuporomoka” (tazama sehemu ya Urithi wa Hawa). Katika Israeli ya
leo, wanawake hawaruhusiwi kutoa ushahidi katika mahakama za kidini. Wanazuoni
wanahalalisha sababu za kutoruhusiwa kwa wanawake kutoa ushahidi kwa kukariri
(Mwanzo 18:9-16), pale ilipoeleza kuwa Sara mke wa Ibrahimu ameongopa.
Wanazuoni wa Kiyahudi wanatumia tukio hili kama ni ushahidi wa kuwa wanawake
hawana vigezo vya kuwa mashahidi. Hapa inapaswa izingatiwe kuwa, kisa hiki
kilichosimuliwa na (Mwanzo 18:9-16) kimetajwa zaidi ya mara moja katika Quran
bila ya kudokeza kama Sara aliongopa (Quran 11:69-74, 51:24-30). Katika Ukristo
wa Kimagharibi, vyanzo viwili Ecclesiastical na sheria ya uraia viliwakataza
wanawake wasitoe ushahidi hadi mwishoni mwa karne iliyopita.
Kama
mwanamume atamuoa mwanamke kisha akamtuhumu kuwa si bikira, ushahidi wa
mwanamke huyo hautokubaliwa. Wazazi wake watalazimika kuleta ushahidi wa
ubikira wake mbele ya wazee wa mji. Na kama wazazi watashindwa kuleta ushahidi
wa kuthibitisha utakatifu wa binti yao, binti huyo atapigwa mawe hadi afe
mlangoni katika ngazi za nyumba ya babaye. Na kama Kama mwanmume atamtuhumu
mkewe kwa uzinzi, ushahidi wa mwanamke huyo hautokubaliwa kabisa kabisa kwa
mujibu wa Biblia. Mke anayetuhumiwa lazima akabiliwe na hukumu ya kuchunguzwa
kwa kuteswa. Katika majaribio hayo, mke atakabiliwa na kanuni za kidini
zikichanganyika na kufedheheshwa ambazo zitapendekezwa ili kuthibitisha uovu wake
au utakatifu wake (Hesabu 5:11-31). Na kama atapatikana na hatia baada ya
kuchunguzwa kimateso, mwanamke huyo atahukumiwa kifo. Na kama itagundulika si
muovu, mumewe atakuwa hana hatia yoyote ya kumtendea vibaya mwanamke huyo.
“Mtu
akitwaa mke, akamwingilia na kumchukia, kisha akimshitaki mambo ya aibu
kumzushia jina baya, akasema, Nimemtwaa mwanamke huyu, nami nilipomkaribia
sikuona kwake alama za ubikira; ndipo babaye yule kijana na mamaye watakapotwaa
alama za yule kijana za ubikira, wawatolee wazee wa mji langoni; na baba yake
yule kijana awaambie wazee, Mwanamume huyu nilimpa binti yangu awe mkewe, naye
amchukia; angalieni amemwekea mambo ya aibu, asema, Sikuona kwa binti yako
alama za ubikira, nazo hizi ndizo alama za binti yangu za ubikira. Na wayakunjue
yale mavazi mbele ya wazee wa mji. Basi wazee wa mji ule na wamtwae yule mtu
mume na kumrudi, wamtoze shekeli mia za fedha, wampe babaye yule kijana, kwa
kuwa amemzulia jina baya mwanamwali wa Israeli; naye awe mkewe; hana ruhusa ya
kumuacha siku zake zote. Lakini likiwa ni kweli neno hili, la kutoonekana kwake
yule kijana alama za ubikira, na wamtoe nje yule kijana mlangoni pa nyumba ya
baba yake, na waume wa mji wake wampige kwa mawe hata afe; kwa vile alivyofanya
upumbavu katika Israel, kwa kufanya ukahaba katika nyumba ya baba yake; ndivyo
utakavyoondo uovu katikati yako (Kumb. 22:13-21).
Uasherati
Uzinzi unazingatiwa kuwa ni dhambi katika dini zote. Biblia inatangaza adhabu ya kifo kwa wote wawili mzinifu mwanamume na mzinifu mwanamke (Law. 20:10). Uislam pia unatoa adhabu iliyo sawa kwa wote wawili mzinifu mwanamume na mzinifu mwanamke (Quran 24:2). Hata hivyo, ufafanuzi wa Quran juu ya uzinzi una tofauti sana na ufafanuzi wa Biblia.
Uzinzi unazingatiwa kuwa ni dhambi katika dini zote. Biblia inatangaza adhabu ya kifo kwa wote wawili mzinifu mwanamume na mzinifu mwanamke (Law. 20:10). Uislam pia unatoa adhabu iliyo sawa kwa wote wawili mzinifu mwanamume na mzinifu mwanamke (Quran 24:2). Hata hivyo, ufafanuzi wa Quran juu ya uzinzi una tofauti sana na ufafanuzi wa Biblia.
Uzinzi,
kwa mujibu wa Quran, ni kushiriki tendo la ngono nje ya ndoa kwa aliyeoa au
aliyeolewa. Lakini Biblia inazingatia tendo la ngono nje ya ndoa kuwa ni uzinzi
kwa mwanamke aliyeolewa. (Law. 20:10, Kum 22:22, Methali 6:20-7:27).
“Akifumaniwa mtu mume amelala na mwanamke aliyeolewa na mume, na wafe wote
wawili, mtu mume alielala na mwanamke, na yule mwanamke naye; ndivyo
utakavyoondoa uovu katika Israeli (Kum 22:22). “Na mtu aziniye na mke wa mtu
mwingine, naam, yeye aziniye na mke wa jirani yake, mtu mume aziniye, na
mwanamke aziniye, hakika watauawa maana wametenda dhambi (Law, 20:10).
Kwa
mujibu wa ufafanuzi wa Biblia, kama mwanamume aliyeoa atalala na mwanamke
asiyeolewa, jambo hilo halichukuliwi kuwa ni uovu kabisa kabisa. Mwanamume
aliyeoa anayefanya ngono nje ya ndoa na mwanamke asiyeolewa si mzinzi na mwanamke
asiyeolewa aliezini naye, pia, si mzinzi. Uovu wa zinaa unatendeka pale tu,
mwanamume aliyeoa au asiyeoa, anapolala na mwanamke aliyeolewa. Kwa hali hii
mwanamume anachukuliwa kuwa ni mzinifu, hata kama hajaoa, na mwanamke
anachukuliwa kuwa ni mzinifu. Kwa ufupi, uzinzi ni uovu wa kingono
unaomuhusisha mwanake aliyeolewa. Matendo ya ngono nje ya ndoa yanayomuhusu
mwanamume aliyeoa si uzinzi kwa mujibu wa Biblia. Je, Kwa nini huu u-ndumilakuwili?.
Kwa mujibu Insaiklopidia ya Kiyahudi, mke anazingatiwa kuwa ni miliki ya mume
na uzinzi unatoa madaraka ya uvunjaji wa sheria kumvunjia mume kwa haki ya
kipekee aliyonayo kwa mwanamke; mke kama miliki ya mume hana haki kama hiyo kwa
mumewe.
Hadi
hivi leo katika nchi ya Israeli, kama mwanamume aliyeoa atajitumbukiza katika
ngono nje ya ndoa na mwanamke asiyeolewa, watoto wake kwa mwanamke huyo
wanazingatiwa kuwa ni watoto wa halali wa ndoa. Lakini, kama mwanamke
aliyeolewa atafanya ngono nje ya ndoa na mwanamume mwingine (si mumewe) aliyeoa
au asiyeoa, watoto wake kwa mwanamume huyo si wa halali tu lakini pia
wanazingatiwa kuwa ni watoto wa haramu na ni haramu kwa watoto huo kuoa au
kuolewa na Myahudi yeyote ispokuwa aliyeitoka dini ya Kiyahudi na watoto wa nje
Hiyo ndio maana, kama mwanamume atafanya ngono na mwanamke aliyeolewa,
mwanamume huyo atakuwa amevunja mali ya mwanamume mwingine na, kwa hiyo lazima
aadhibiwe (Jeffrey, 1990:170-177). Katazo hili linaendelea kwa vizazi vya mtoto
huyo kwa madaraja ya vizazi mpaka uvundo wa uzinzi uthibitishwe kufifia (Quran
41-42). Kwa upande mwingine,
Kula
Kiapo na Kuweka Nadhiri
Nadhiri
au kiapo cha mwanamke lazima kitimizwe na baba yake, kama atakuwa anaishi
kwenye nyumba ya baba yake, au atimiziwe na mumewe, akiwa ameolewa. Kama
baba/mume hajaidhinisha nadhiri ama kiapo cha binti yake au mkewe, viapo,
ahadi, nadhiri na dhamana zote zilizofanywa na mwanamke huyo zinakuwa ni batili
na ni kazi bure: “Lakini kama huyo baba yake akimkataza siku hiyo aliyosikia;
nadhiri zake ziwazo zote, wala vifungo vyake alivyoifungia nafsi yake
havitathibitika….” Na mumewe alisikia akamnyamazia, wala hakumkataza; ndipo
nadhiri Zake zote zitathibitika na kila kifungo alichofunga kitathibitika.
(Hesabu 30:5-15). Kwa nini iwe maneno ya mwanamke hayashurutishwi kwake? Jibu
ni lepesi: Ni kwa sababu mwanamke anamilikiwa na baba yake, kabla ya kuolewa,
au na mumewe baada ya kuolewa. Utawala wa baba kwa binti yake ulikuwa ni
dhahiri kwa upeo ambao, kama atataka, anaweza kumuuza! Na jambo hilo
limeonyeshwa katika maandiko ya wanazuoni wa Kiyahudi kuwa: “Mwanamume anaweza
kumuuza binti yake, lakini mwanamke hawezi kumuuza binti yake, Mwanamume
anaweza kumchumbia binti yake, lakini mwanamke hawezi.”
Kushindwa
kutekeleza kiapo ipasavyo, kilichoapwa na mwanamume au mwanamke, ni lazima
alipe fidia kama ilivyotajwa katika Quran: “Mwenyezi Mungu hatakuteseni kwa
viapo vyenu vya upuuzi, lakini Atakukamateni kwa viapo mlivyoapa kwa nia
mliyoifunga barabara. Basi kafara yake ni kuwalisha masikini kumi kwa chakula
cha katikati mnachowalisha watu wa majumbani mwenu, au kuwavisha, au kumpa
uungwana mtumwa, Lakini asiyeweza kupata hayo, basi afunge siku tatu (Quran
5:89). Wafuasi wa Mtume Muhammad (S.A.W) waume kwa wake, walikuwa wakiwasilisha
viapo vyao vya kumtii, wao wenyewe. Wanawake, sawa na wanaume, walikuwa wanamuendea
Mtume kila mtu mwenyewe na kula viapo vyao. “Ewe Nabii! Watakapokujia wanawake
walioamini wanakuahidi ya kwamba hawatamshirikisha Mwenyezi Mungu na chochote,
wala hawataiba, wala hawatazini, wala hawatawaua watoto wao, wala hawataleta
uzushi wanaouzusha tu wenyewe baina ya mikono yao na miguu yao, wala
hawatakuasi katika jambo jema, basi peana ahadi nao na uwatakie maghufira kwa
Mwenyezi Mungu.
Mali
za Mwanamke
Mafundisho
ya Kiyahudi yanalichukulia jukumu la mume kwa mkewe kuwa linaanzia kutoka
katika itikadi ya kuamini kuwa mume anammiliki mke kama anavyomiliki mtumwa
wake. Itikadi hii imekuwa hoja nyuma ya undumilakuwili katika sheria ya uzinzi
na nyuma ya uwezo wa mwanamume wa kubatilisha viapo vya mkewe. Itikadi hii pia
inahusika katika kumzuia mke asisimamie mali yake au mapato yake. Mwanamke wa
Kiyahudi mara tu anapoolewa, mwanamke huyo anapoteza kabisa kabisa usimamizi wa
mali zake na mapato yake, na kuchukuliwa na mumewe. Wanazuoni wa Kiyahudi
wanatetea haki ya mwanamume kwa mali ya mkewe kama ni matokeo ya kummiliki
kwake mke huyo: “Mtu anapokuwa mmiliki wa mwanamke je, jambo hilo halipelekei
kuwa mtu huyo atakuwa mmiliki wa mali za mwanamke huyo vile vile?” na “Na
mwanamume ajitwalie mwanamke je, hatajitwalia mali za mwanamke huyo vile vile? Ukweli
wa mambo ni kwamba mali za mwanamke wa Kiyahudi zina maana ya kuwavutia
wachumba.
Familia
ya Kiyahudi inatoa fungu la binti yao katika kiwanja/shamba la baba yake
litumiwe kama mahari atoayo mke ili aolewe. Mahari hiyo ndiyo sababu iliyowafanya
mabinti wa Kiyahudi wewe ni balaa lisilotakiwa kwa baba zao. Baba analazimika
kumlea binti yake kwa miaka mingi kisha aandae ndoa yake kwa kutoa mahari
kubwa. Kwa hiyo, msichana katika familia ya Kiyahudi amekuwa ni dhima isiyo na
kikomo na sio rasilimali.Kwa hiyo, ndoa imesababisha mwanamke tajiri sana awe
hana kitu! Talmudi inachambua hali ya kiuchumi ya mwanamke kama ifuatavyo:
“Vipi mwanamke awe na chochote; chochote ambacho ni chake kinamilikiwa na
mumewe? Kwa mume kile ambacho ni chake basi hicho ni chake na kwa mwanamke kile
ambacho ni chake basi hicho ni cha mwanamume vile vile. Ni lazima iongezwe kuwa
mume vile vile analazimika atoe mahari kwa bibi harusi, lakini kwa mara
nyingine tena mume huyo huyo ndio mmiliki halali wa zawadi hiyo kwa muda wote
wa ndoa yao.
Ukristo,
hadi hivi karibuni, umekuwa unafuata mafundisho yale yale ya Kiyahudi. Mamlaka
za sheria za raia katika himaya ya Ukristo wa Kiroma (baada ya Constantine)
zinaomba maafikiano ya mali kama ni sharti la kutambuliwa kwa ndoa. Familia
zinawapa mabinti zao mahari za ziada kama matokeo ya sheria hiyo. Chini ya
sheria ya urai, mke ametajwa kuwa anarudishiwa mahari yake kama ndoa
imebatilishwa, ila kama mwanamke huyo ni mzinzi, katika hali hii, mwanamke huyo
ananyang`anywa haki yake ya mahari ambayo imesalia kuwa mikononi mwa mumewe.24
Chini ya sheria ya kanuni na sheria ya uraia mwanamke aliyeolewa katika dini ya
Ukristo wa Ulaya na Marekani ameshapoteza haki za mali zake, hali hii ilikuwa
inaendelea hadi mwishoni mwa karne ya kumi na tisa na mwanzoni mwa karne ya
ishirini. Kwa mfano, haki za wanawake chini ya sheria ya Uingereza zilizotungwa
na kuchapishwa 1632. Miongoni mwa haki hizo ni: “Cha mume ni chake.
Mke
sio tu anapoteza mali zake katika ndoa, pia anapoteza utu wake. Mumewe anaweza
kubatilisha uuzaji au zawadi iliyotolewa na mke kwa kuwa haina sharti lenye
thamani kisheria. Mtu yeyote atakayeingia mkataba na mke wa mtu anachukuliwa
kuwa ni haramia kwa kushiriki katika ulaghai. Zaidi ya hayo, mwanamke hawezi
kushtaki au kushtakiwa kwa jina lake mwenyewe, wala hawezi kumshitaki mumewe.
Mwanamke aliyeolewa alikuwa anatendewa kama vile ni mtoto mchanga katika jicho
la sheria. Kirahisi kabisa, mke alimilikiwa na mumewe na kwa hiyo anapoteza
mali zake, utu wake kisheria, na jina lake la kifamilia.
Mali
na pato la mke vipo chini ya utawala wake kikamilifu na ni kwa ajili ya
matumizi yake peke yake, na mutumizi ya watoto, ni jukumu la mumewe. Quran
imeelezea msimamo wake juu ya mada hii kwa uwazi kabisa: “Na wapeni wanawake
mahari yao, hali ya kuwa ni hadiya (aliyowapa Mungu). (Lakini hao wake zenu)
wakikupeni kwa radhi ya nafsi zao kitu katika hayo (mahari) basi kuleni kwa
furaha na kunufaika. (Quran 4:4). Bila kujali huyo mke ni tajiri kiasi gani,
mwanamke halazimishwi kuwa mchumiaji mwenza wa mwanamume kuihudumia familia
ispokuwa kama atajitolea mwenyewe na kuamua kufanya hivyo.
Talaka
Hizi dini tatu zina tofauti zilizo wazi kimtazamo juu ya talaka ambapo Ukristo unapinga talaka moja kwa moja. Agano Jipya kwa kauli moja linapigania ndoa isiyotanguka. Inasemekana kuwa Yesu amesema: “Lakini mimi nawaambia, kila mtu amwachaye mkewe, ispokuwa kwa habari ya uasherati, amfanya kuwa mzinzi; na mtu akimwoa yule aliyeachwa, azini. (Matayo 5:32). Ukamilifu huo ulio mgumu kutekelezeka na usiobadilika bila ya shaka si jambo la hakika. Jambo hilo linaibua dhana ya ukamilifu wa kimaadili ambao haufikiwi na jamii ya kibinadamu. Wakati wanandoa wanapogundua kuwa ndoa yao haiwezi kuendelea, tendo la kuharamisha talaka haliwatendei wema wowote wanandoa hao. Kuwalazimisha wanandoa wanaochukiana waishio kwa ubaya wakae pamoja kinyume na matakwa yao ni jambo lisilo na maana yeyote wala si la haki.
Hizi dini tatu zina tofauti zilizo wazi kimtazamo juu ya talaka ambapo Ukristo unapinga talaka moja kwa moja. Agano Jipya kwa kauli moja linapigania ndoa isiyotanguka. Inasemekana kuwa Yesu amesema: “Lakini mimi nawaambia, kila mtu amwachaye mkewe, ispokuwa kwa habari ya uasherati, amfanya kuwa mzinzi; na mtu akimwoa yule aliyeachwa, azini. (Matayo 5:32). Ukamilifu huo ulio mgumu kutekelezeka na usiobadilika bila ya shaka si jambo la hakika. Jambo hilo linaibua dhana ya ukamilifu wa kimaadili ambao haufikiwi na jamii ya kibinadamu. Wakati wanandoa wanapogundua kuwa ndoa yao haiwezi kuendelea, tendo la kuharamisha talaka haliwatendei wema wowote wanandoa hao. Kuwalazimisha wanandoa wanaochukiana waishio kwa ubaya wakae pamoja kinyume na matakwa yao ni jambo lisilo na maana yeyote wala si la haki.
Si
ajabu ulimwengu wa Wakristo wote unalazimisha kuruhusiwa kwa talaka. Wayahudi,
kwa upande mwingine, wanaruhusu talaka hata ikiwa bila sababu. Agano la kale
linampa mume haki ya kumtaliki mkewe hata kama hana kosa au kwa kuwa hampendi
tu. “Mtu akiisha kutwaa mke kwa kumwoa, asipopata kibali machoni mwake, kwa
kuwa ameona neno ovu kwake, na amwandikie hati ya kumwacha, akamtilie mkononi
mwake na kumtoa katika nyumba yake. Naye akiisha kuondoka katika nyumba yake,
ana ruhusa kwenda akawa mke wa mtu mwingine. Na huyo mumewe wa sasa akimchukia,
na kumwandikia hati ya kumwacha, na kumpa mkononi mwake, na kumtoa katika
nyumba yake; au akifa yeye mumewe wa sasa, aliyemtwaa kuwa mkewe; yule wa
kwanza aliyemwacha asimtwae kuwa mkewe tena, akiisha kutiwa unajisi; kwa kuwa
haya ni machukizo mbele za BWANA; kwa hiyo asiitie dhambini nchi, akupayo
BWANA, Mungu wako, iwe urithi.” (Kum 24:1-4) Aya iliyo hapo juu imesababisha
mjadala mkali kwa Wanazuoni wa Kiyahudi kwa sababu ya kutokubaliana kwao juu ya
tafsiri ya maneno. “Uovu, chuki, kutia aibu, tabia mbaya” na “kutopenda”
yaliyotajwa katika hizo aya. Kitabu cha Talmudi kinasajili rai zao
zilizotofauti tofauti: “Madhehebu ya Shamai inakamata kuwa mwanamume haruhusiwi
kumwacha mkewe ila kama atampata na hatia ya uzinifu, huku madhehebu ya Hillel
yanasema kuwa mwanamume anaweza kumwacha mkewe hata kama huyo mwanamke amevunja
kibakuli cha mumewe. Na mwanazuoni Akiba anasema mwanamume anaweza kumwacha mke
hata kama kwa sababu nyepesi ya kwamba amempata mwanamke mwingine aliyemzuri
sana kuliko wa kwanza” (Gittin, 90a-b).
Agano
Jipya linafuata rai ya Shamaites huku sheria ya Kiyahudi imefuata rai ya
(Hillelites & Akiba, 1962). Tangu kuenea kwa rai ya Hillelites, imekuwa ni
mafundisho yasiyokeukwa kwa sheria ya Wayahudi ya kuwapa uhuru wanaume wa
kumuacha mkewe bila ya sababu yoyote. Agano la Kale sio tu linampa mume haki ya
kumtaliki mkewe “aliyemuhuzunisha” lakini pia linazingatia kumwacha “mke muovu”
ni lazima: “Mke mbaya analeta fedheha, muono wa kuhuzunisha, na maumivu ya
moyo. Mgoigoi wa mkono na mdhaifu wa goti ni mwanamume ambaye mkewe ameshindwa
kumfurahisha. Mwanamke ni dhambi ya asili, na kupitia kwake sote tutakufa.
Usiache tangi lenye ufa kuchimba au kumruhusu mke mbaya asema atakacho. Na kama
mwanamke huyo hakubali utawala wake, mwache na mfukuze.” (Ecclesiasticus
25:25). Talmudi imesajili matendo maalumu kadhaa ya wake wanaolazimika kuachwa
na waume zao: “Kama mwanamke atakula mitaani, kama atakunywa kwa pupa mitaani,
kama atanyonyesha mtaani, kwa matendo hayo yote mwanazuoni Meir amesema kuwa
mwanamke huyo lazima aachane na mumewe” (Git. 89a). Vile vile Talmudi imefanya
jambo hilo kuwa ni mamlaka ya kumuacha mwanamke mgumba (ambaye hazai kwa
kipindi cha miaka kumi): “Mwanazuoni wetu ametufundisha: Kama mwanamume
amejitwalia mke na kuishi nae kwa miaka kumi na mwanamke huyo hajazaa mtoto,
mwanamume huyo amuache mke huyo” (Yeb. 64a).
Wake,
kwa upande mwingine, hawawezi kutoa talaka chini ya ya sheria ya Kiyahudi. Mke
wa Kiyahudi, hata hivyo, anaweza kuomba talaka mbele ya mahakama ya Kiyahudi
huku akithibitisha sababu nzito ya kufanya hivyo. Ni nafasi ndogo sana apewayo
mke ili aweze kuomba talaka. Miongoni mwa nafasi hizo ni: ikiwa mumewe ana
ugonjwa mbaya au ugonjwa wa ngozi, mumewe akishindwa kutekeleza wajibu wa ndoa.
Hiyo mahakama inaweza kuunga mkono madai ya mke ya kutaka talaka lakini haina
uwezo wa kuvunja ndoa. Ni mume tu awezaye kuvunja ndoa kwa kumtoza mkewe faini
ya talaka. Na mahakama inao uwezo wa kutoa adhabu ya viboko, faini, kifungo na
kumtenga na sinagogi huyo mume ili kumlazimisha apokee malipo ya lazima ya
kumtaliki mkewe. Hata hivyo, kama mume atakuwa mbishi vya kutosha, anao uwezo
wa kutotoa talaka na kuendelea kubaki na mkewe bila ya mipaka. Na baya zaidi,
ni kuwa, mume anao uwezo wa kumtelekeza mkewe bila ya kumpa talaka na kumuacha
akiwa si mwolewa wala si mtalikiwa. Na huyo mume anaweza kuoa mke mwingine au
hata kuishi na kimada bila ya ndoa na kupata watoto kwa huyo kimada, (watoto
hao wanahesabiwa kuwa ni wa halali katika sheria za Kiyahudi). Mke
aliyetelekezwa, kwa upande mwingine, haruhusiwi kuolewa na Myahudi mwingine,
kwa kuwa yeye ni mke wa mtu kisheria na hawezi kuishi na mwanamume mwingine kwa
sababu atahesabiwa kuwa ni mzinifu na watoto wake kwa huyo mwanamume mwingine
pia si wa halali kwa vizazi kumi.
Mwanamke
mmoja alimuendea Mtume Muhammad (S.A.W) akitaka kuvunjwa kwa ndoa yake,
akamwambia Mtume kwamba yeye hana lalamiko lolote dhidi ya tabia au hali ya
mumewe. Tatizo lake la pekee lilikuwa ni kuwa hampendi huyo Kama mume atavunja
ndoa kwa kumtaliki mkewe, hatorudishiwa chochote miongoni mwa mahari aliyotoa
kumpa mkewe. Quran imeeleza kuharamisha kwa mume aliyeacha mke asirudishiwe
mahari bila kujali ughali au thamani ya mahari yenyewe: “Na kama mkitaka
kubadilisha mke mahali pa mke, (yaani kumwoa mke mwingine na kumwacha huyo wa
zamani), na hali mmoja wao (nae ndiye huyo anayemwacha) mumempa mrundi wa mali,
basi msichukue chochote. Je, mnachukua kwa dhulma na kwa khatia iliyo wazi?”
(Quran 4:20). Katika hali ya mke kuamua kumaliza ndoa, huyo mke anatakiwa
arejeshe mahari kwa mumewe. Kurejesha mahari katika hali hii ni fidia ya
uadilifu kwa mume ambaye anapendelea kuendelea na mkewe huku huyo mke anataka
waachane. Quran imewafundisha waume wa Kiislamu wasichukue kitu chochote katika
mahari walizowapa wake zao ispokuwa katika hali ya mke kuamua kuvunja ndoa:
“…Wala si halali kwenu kuchukua chochote mlichowapa (wake zenu), ispokuwa (wote
wawili) wakiogopa ya kwamba hawataweza kusimamisha mipaka ya Mwenyezi Mungu”.
Uislamu
umempa mwanamke wa Kiislamu baadhi ya haki (chache): mwanamke anaweza kumaliza
ndoa kupitia khulah na kufungua mashitaka ya kudai talaka. Mke wa Kiislamu
kamwe hatokuwa mtundikwa na mume mkaidi. Na zilikuwa ni haki hizi
zilizowashawishi wanawake wa Kiyahudi waliokuwa wakiishi katika jamii za
Kiislamu za mwanzo za karne ya 7 C.E. watafute kupata malipo ya talaka kutoka
kwa waume zao wa Kiyahudi kupitia mahakama za Kiislamu. Wanazuoni wa Kiyahudi
walitangaza kuwa malipo hayo ni batili na hayafai. Ili kukomesha mwenendo huo,
wanazuoni wa Kiyahudi walitoa haki mpya na marupurupu kwa wanawake wa Kiyahudi
ili kujaribu kudhoofisha mvuto wa mahakama za Kiislamu. Wanawake wa Kiyahudi
waishio katika nchi za Kikristo hawakupewa chochote katika marupurupu kama yale
ya wenzao. Kwa kuwa sheria ya talaka ya Kirumi inayofanyakazi ilikuwa haina
mvuto wa ziada kuliko sheria za Kiyahudi. Vile vile, Mtume, amesisitiza kuwa
Waislamu wabora sana ni wale walio wabora kwa wake zao: Sasa, hebu acha
tutazame namna Uislamu usivyopendelea talaka. Mtume wa Uislamu amewaambia
waumini kuwa: “Jambo la halali linalomchukiza sana Mwenyezi Mungu ni talaka.”
Mwanamume
wa Kiislamu hatakiwi kumtaliki mkewe eti kwa kuwa hampendi. Quran inawafundisha
wanaume wa Kiislamu wawe wema kwa wake zao hata katika hali ya hisia za
kuvuvuwaa au hisia za kutompenda: “….Na kaeni nao kwa wema; na kama mkiwachukia
basi (msiwaache) kwani huenda mkakichukia kitu, na Mwenyezi Mungu ametia kheri
nyingi ndani yake. (Quran 4:19) Mtume Muhammad (S.A.W) ametoa mafundisho kama
hayo: “Muumini wa kiume asimchukie muumini wa kike, kama hapendi moja ya tabia
zake atapendezwa na nyinginezo” (Muslim) (David, 1896:125-126). “Mkamilifu wa
imani miongoni mwa waumini ni yule mbora wao kitabia na aliye mbora wenu
kitabia ni yule mwenye tabia njema kwa mkewe.” (Tirmidhi) Hata hivyo, Uislamu
ni dini ya vitendo na inatambua kuwa kuna wakati ndoa inakuwa ipo ukingoni
karibu kuvunjika. Na kama mkijua kuwa kuna ugomvi baina ya mke na mume basi
pelekeni mwamuzi mmoja katika jamaa za mwanamume na mmoja katika jamaa za
mwanamke. Hakika Mwenyezi Mungu ni mjuzi wa habari za siri na habari za dhahiri
(Quran 4:34-35).
Mambo
matatu ya kwanza kutajwa yajaribiwe kwanza. Na kama yameshindwa, ndipo
inapotakiwa kutafutwa msaada wa familia. Ni lazima izingatiwe, kuwa aya za hapo
juu zinaangaza, kuwa kumpiga mke mkaidi, ni kipimo cha muda mfupi ambacho
kinakimbiliwa kikiwa ni hatua ya tatu tena katika hali ya kulazimika kufanya
hivyo huku kukiwa na matarajio ya kuwa hiyo itakuwa dawa ya matendo maovu ya
mke. Kama hilo litafaa, basi mume haruhusiwi kwa hali yoyote ile kuendelea
kumsumbua mke kama ilivyotajwa kwa ufafanuzi katika aya hizo. Na kama njia hiyo
imeshindwa, mume bado haruhusiwi kutumia tena njia hiyo na hapo ndipo njia ya
mwisho ya suluhisho kwa msaada wa familia lazima iangaliwe.
Kwa
kuongezea, Mtume wa Uislamu amelaani mapigo yoyote yasiyo ya kiuadilifu. Baadhi
ya wake wa Kiislamu walimshitakia Mtume (S.A.W) kuwa waume zao wamewapiga. Kwa
kusikia hivyo, Mtume kwa dhahiri alisema kuwa: “Wale wafanyao hayo (kuwapiga
wake zao) si wabora wenu.
Akina
Mama
Agano
la Kale katika sehemu nyingi linaamrisha wema na kutenda matendo ya pekee kwa
wazazi na kuwalaani wale ambao hawawatendei wema. Kwa mfano, “Kwa maana kila
mtu amlaaniye baba yake au mama yake hakika atauawa; amemlaani baba yake na
mama yake; damu yake itakuwa juu yake.” (Mambo ya walawi 20:9) “…Mwana mwenye
hekima humfurahisha babaye; bali mpumbavu humdharau mamaye.” (Mithali 15:20).
Ingawa kumfanyia wema baba peke yake ndiko kulikotajwa katika baadhi ya sehemu;
kwa mfano, “Mwana mwenye hekima husikiliza mausia ya babaye; Bali mwenye dharau
hasikilizi maonyo” (Mithali 13:1). Mama peke yake ndiye asiyetajwa. Zaidi ya
hayo, hakuna msisitizo wa kipekee juu ya kumtendea wema mama kama alama ya
kufahamu vizuri tabu nyingi alizozipata wakati wa kujifungua na matatizo ya
mtoto mchanga. Kando ya hayo, akina mama hawarithi kabisa kabisa chochote toka
kwa watoto wao huku akina baba wanarithi mali. Huu ni uonevu na tafsiri yake ni
kwamba mke hazalishi.
Mtu
anaweza akadai kuwa Yesu alikuwa akijaribu kuwafundisha makutano yake somo
muhimu sana ambalo ni kuwa uhusiano wa kidini si wenye umuhimu mdogo kuliko
uhusiano wa kifamilia. Hata hivyo, Yesu alikuwa na uwezo wa kuwafundisha
wasikilizaji wake somo hilo hilo bila ya kuonyesha huko kutomjali mama yake Ni
vigumu kusema kuwa Agano Jipya ni maandiko yanayowataka watu wawafanyie wema akinamama.
Kwa kulinganisha, mtu anaona kuwa Agano Jipya linahesabu kuwatendea wema
akinamama kuwa ni kikwazo katika njia ya Mwenyezi Mungu. Kwa mujibu wa Agano
Jipya, mtu hawezi kuwa Mkristo mzuri wa kutumainiwa kuwa yeye ni mfuasi wa
Kristo ila amchukie mama yake. Inasemekana kuwa Yesu alisema: “Kama mtu akija
kwangu naye hamchukii baba yake, na mama yake, na mke wake, na wanawe, na ndugu
zake waume na wake; naam na hata nafsi yake mwenyewe, hawezi kuwa mwanafunzi
wangu.” (Luka 14:26) Kwa kuongezea, Agano Jipya linatoa picha ya Yesu kama ni
mtu mwenye tofauti au asiyemuheshimu mama yake mzazi. Kwa mfano, wakati mama
yake alipokwenda kumtafuta na huku Yesu akiwa anawahubiria makutano, Yesu
hakujali wala hakutoka kwenda kumuona mama yake: “Wakaja mamaye na nduguze;
wakasimama nje, wakatuma mtu kumwita. Na makutano walikuwa wameketi,
wakimzunguka; wakamwambia, Tazama, mama yako na ndugu zako wako nje,
wanakutafuta. Akawajibu, akisema, Mama yangu na ndugu zangu ni akina nani?
Akawatazama wale walioketi wakimzunguka pande zote, akasema, Tazama, mama yangu
na ndugu zangu! Kwa maana mtu ye yote atakayeyafanya mapenzi ya Mungu, huyo
ndiye ndugu yangu, na umbu langu, na mama yangu” (Marko 3:31-35). Mwelekeo kama
huo usio na heshima unatoa picha ya wakati alipokataa kuthibitisha maelezo
yaliyotolewa na makutano yake ya kuibariki kazi ya mama yake ya kumzaa na
kumlea: “Ikawa alipokisema maneno hayo, mwanamke mmoja katika mkutano alipaza
sauti yake, akamwambia, Heri tumbo lililokuzaa, na matiti uliyonyonya. Lakini
yeye alisem, Afadhali, heri walisikiao neno la Mungu na kulishika” (Luka
11:27-28). Ikiwa mama mwenye daraja ya bikira Maria ametendewa matendo yasio na
heshima kiasi hicho, kama ilivyofafanuliwa na Agano Jipya, tena katendewa na
mtoto mwenye daraja ya Yesu Kristo, sasa itakuwaje kwa mama wa kawaida wa
Kikristo vipi atatendewa na wanawe wa Kikristo wa kawaida? Katika Uislamu,
heshima, utiifu, na kutukuza kunaambatana na mfano ambao hauna kifani.
Quran
inaweka umuhimu wa kuwatendea wema wazazi kuwa ni jambo la pili baada ya
kumuabudu Mwenyezi Mungu Muweza: “Na Mola wako amehukumu kuwa msimuabudu yoyote
ila Yeye tu. Na (ameagiza) kuwafanyia wema (mkubwa) wazazi. Kama mmoja wao
akifikia uzee, (naye yuko) pamoja nawe, au wote wawili, basi usiwaambie hata
Ah! Wala usiwakemee. Na useme nao kwa msemo wa hishima (kabisa). Na
uwainamishie bawa la unyenyekevu kwa (njia ya kuwaonea) huruma (kwa kuwaona
wamekuwa wazee). Na useme; “Mola wangu! Warehemu (wazee wangu) kama
walivyonilea katika utoto.” (Quran 17:23-24) Quran katika sehemu kadhaa imeweka
mkazo maalumu kwa kazi ya mama ya kuzaa na kulea: “Na tumemuusia mwanadamu
(kuwafanyia ihsani) wazazi wake – mama yake ameichukuwa mimba yake kwa udhaifu
juu ya udhaifu, na (kumnyonyesha na kuja) kumwachisha kunyonya katika miaka miwili
– ya kwamba unishukuru mimi na wazazi wako; marejeo yenu ni kwangu,” (Quran
31:14) Nafasi ya pekee ya akina mama katika Uislamu imeelezwa kwa umbuji
(ufundi wa kupanga na kutumia maneno kwa ujuzi wa hali ya juu sana) na Mtume
Muhammad (S.A.W): “Mtu mmoja alimuuliza Mtume: “Ni nani nimfanyie wema zaidi?
Mtume (S.A.W) akamjibu: “Mama yako”. “Na nani anafuata?” Aliuliza yule jamaa.
Mtume (S.A.W) akamjibu: “Mama yako”. “Na nani anafuata?” Aliuliza yule jamaa
Mtume (S.A.W) akamjibu: “Mama yako”.
Mirathi
kwa Wanawake
Moja
ya tofauti kubwa kati ya Quran na Biblia ni mitazamo yao juu ya mirathi ya
wanawake kurithi mali za ndugu zao waliofariki. Mtazamo wa Kibiblia una maneno
mafupi yaliyowazi na yalioelezwa na mwanazuoni Epstein: “Mafundisho
yanayoendelea na yasiyovunjika tangu enzi za kuanza Biblia hayampi mwanamke,
mke na mabinti haki ya kurithi mali ya familia. Katika mfumo mkongwe sana wa
urithi, wanafamilia wa kike wanazingatiwa kuwa ni sehemu ya mali ya urithi na
kuwa ni watu wa mbali kabisa na utu, kisheria wanarithiwa na kuwa wao ni kama
watumwa. Wakati ambapo kanuni za Musa zinatoa mirathi kwa mabinti ikiwa hakuna
mwanaumume. Lakini hata hivyo mke harithi hata katika hali kama hiyo. Kwa nini wanafamilia wa kike wanachukuliwa
kuwa ni sehemu ya urathi? Mwanazuoni Esptein ana jibu: “Wanawake ni miliki ya
baba zao kabla ya kuolewa na ni miliki ya waume zao baada ya kuolewa.”
Ukristo umekuwa ukifuata sheria hizo hizo kwa muda mrefu. Sheria zote mbili za kikanisa na za kiraia kwa Wakristo zinazuia mabinti wasishirikiane na kaka zao katika urithi kutoka kwa baba yao. Kando ya hayo, wake walikuwa wananyimwa haki zote za kurithi. Sheria hiyo ya udhalimu sana ilidumu hadi mwishoni mwa karne iliyopita. Sheria za mirathi za Biblia zimeelezwa katika (Hesabu 27:1-11). Mke hapewi fungu lolote katika mirathi ya mumewe, huku huyo mume ndio mrithi wa kwanza wa kumrithi mkewe, tena hata kabla ya watoto wake. Binti anaweza kurithi kama tu hakuna mwanamume wa kurithi. Mama harithi kabisa kabisa huku baba akirithi. Wajane na mabinti, katika hali ya kuwepo watoto wa kiume, wamo katika huruma ya warithi wa kiume kwa kusaidiwa. Na hiyo ndiyo sababu wajane na mayatima wa kike wamekuwa ni miongoni mwa mafukara sana katika jamii ya Kiyahudi hapo kale.
Ukristo umekuwa ukifuata sheria hizo hizo kwa muda mrefu. Sheria zote mbili za kikanisa na za kiraia kwa Wakristo zinazuia mabinti wasishirikiane na kaka zao katika urithi kutoka kwa baba yao. Kando ya hayo, wake walikuwa wananyimwa haki zote za kurithi. Sheria hiyo ya udhalimu sana ilidumu hadi mwishoni mwa karne iliyopita. Sheria za mirathi za Biblia zimeelezwa katika (Hesabu 27:1-11). Mke hapewi fungu lolote katika mirathi ya mumewe, huku huyo mume ndio mrithi wa kwanza wa kumrithi mkewe, tena hata kabla ya watoto wake. Binti anaweza kurithi kama tu hakuna mwanamume wa kurithi. Mama harithi kabisa kabisa huku baba akirithi. Wajane na mabinti, katika hali ya kuwepo watoto wa kiume, wamo katika huruma ya warithi wa kiume kwa kusaidiwa. Na hiyo ndiyo sababu wajane na mayatima wa kike wamekuwa ni miongoni mwa mafukara sana katika jamii ya Kiyahudi hapo kale.
Akina
mama, wake, wasichana na madada wa Kiislamu wamepokea haki za kurithi miaka
elfu moja na mia tatu kabla ya Ulaya kutambua kuwepo kwa haki hiyo. Mgawo wa
urithi ni somo kubwa sana lenye maelezo kamili katika (Quran 4:7, 11, 12, 176).
Sheria mama ni kuwa fungu la mwanamke ni sawa sawa na nusu ya Miongoni mwa
wapagani wa Kiarabu kabla ya Uislamu, haki za kurithi zilikuwa kwa ndugu wa
kiume tu. Quran imekomesha dhuluma zote hizo za kiutamaduni na ukawapa ndugu
wote wa kike mafungu ya kurithi: “Wanaume wana sehemu katika mali wanayoyaacha
wazazi na jamaa waliokaribia. Na wanawake (pia) wanayo sehemu katika yale
waliyoyaacha wazazi na jamaa waliokaribia. Hizi ni sehemu zilizofaridhiwa na Mwenyezi
Mungu katika (Quran 4:7) “…mwanamume ispokuwa katika hali ambazo mama anapata
sawa sawa na baba” Hii sheria mama kama itachukuliwa kwa kutengwa kutoka katika
sheria nyinginezo zinazowahusu wanaume na wanawake inawezekana kuonekana kuwa
haina uadilifu. Ili kufahamu uwiano uliopo katika sheria hii, mtu lazima
azingatie ukweli kwamba mujukumu ya kipesa kwa wanaume katika Uislamu yanazidi
sana yale ya wanawake (Tazama kitengo cha mali za wanawake). Mume lazima ampe
mkewe mali. Mahari hiyo ni mali ya huyo mke na inaendelea kuwa hivyo hivyo hata
kama ataachwa hapo baadaye. Bi harusi hana wajibu wa kutoa kitu cha kumpa bwana
harusi. Zaidi ya hayo, mume wa Kiislamu anachajiwa huduma za mkewe na wanawe.
Mke, kwa upande mwingine, halazimishwi kumsaidia mumewe katika majukumu haya.
Mali na pato la mke ni kwa ajili yake binafsi ila kile atakachojitolea kumpa
mumewe. Kando ya hayo, mtu lazima atambue kuwa Uislamu kwa juhudi kubwa
unahimiza maisha ya kifamilia.
Wajane
Kwa
sababu ya ukweli kwamba Agano la Kale halitambui haki yoyote kwa wanawake,
wajane wamekuwa ni miongoni mwa watu masikini sana katika jamii ya Kiyahudi.
Ndugu wa kiume ambao wamerithi mali yote ya mume aliyefariki ambayo ilikuwa
apewe huyo mke kutoka katika mali hiyo. Hata hivyo, wajane hawana jinsi ya
kujihakikishia matumizi hayo ambayo yameshasombwa, na wanaishi kwa kungojea
huruma za watu wengine. Kwa hiyo wajane wamekuwa ni watu wa daraja la chini mno
katika Israeli ya zamani na ujane ulizingatiwa kuwa ni alama ya kushuka hadhi
sana (Isaya 54:4). Lakini hali mbaya ya mjane katika mafundisho ya Kibiblia
inaenea hadi nga`mbo ya kutengwa kutoka katika mali ya mumewe. Kwa mujibu wa
Mwanzo 38, mjane asiye na mtoto lazima aolewe na ndugu wa mumewe, hata kama
atakuwa ameshaoa, kwa hiyo huyo ndugu azae mtoto kwa ajili ya kaka yake
aliyefariki, jambo ambalo litaimarisha jina la ndugu yake na halitokufa. “Yuda
akamwambia Onani, uingie kwa mke wa nduguyo ukamwoe, ukamwinulie nduguyo uzao”
(Mwanzo 38:8). Radhi za mjane kuridhia ndoa hiyo hazihitajiki. Mjane anatendewa
kama ni sehemu ya mali ya mumewe aliyefariki, mke ambaye faida yake kuu ni
kuhakikisha kizazi cha mumewe. Hii sheria ya Kibiblia bado inatumiwa katika
Israeli ya leo. “Naye atamwoa mwanamke katika ubikira wake. Asitwae mjane, wala
mwanamke aliyeachwa na mumewe, wala mwanamke mwenye unajisi, wala kahaba;
lakini atamwoa mwanamwali katika watu wake mwenyewe. Naye asiwatie unajisi
kizazi chake katika watu wake; kwa kuwa mimi ndimi BWANA nimtakasaye” (Walawi
21: 13-15).
Quran
kwa ukali imeshambulia na kutokomeza mila hii ya kudhalilisha: “Wala msiwaoe
wake waliowaoa baba zenu; ispokuwa yale yaliokwisha pita (Yaliyopita yamepita
yasirejeshwe tena). Bila ya shaka jambo hili ni uovu na uchukizo na ni njia
mbaya.” (Quran 4:22) Wajane na wanwake walioachwa wanadhalilishwa sana katika
itikadi ya Kiyahudi kiasi ambacho Kuhani Mkuu hakuruhusiwa kumuoa mjane,
mtalikiwa, au malaya: Quran kwa upande mwingine, haimchukulii mtu yeyote kuwa
ni wa bahati wala ni wa mikosi. Wajane na watalikiwa wana uhuru wa kuolewa na
mwanamume yeyote wamtakaye. Hakuna aibu inayomkumba mtalikiwa au mjane katika
Quran: “Na mtakapowapa wanawake talaka, nao wakafikia kumaliza eda yao, basi
warejeeni kwa wema au tokaneni nao kwa wema. Wala msiwaweke kwa kuwapa dhara
mkaruka mipaka. Na atakayefanya hivyo, amejidhulumu mwenyewe. Wala msizifanyie
mzaha Aya za Mwenyezi Mungu. Na mkumbuke neema za Mungu zilizo juu yenu, na
(khasa ile neema ya) kuteremshiwa Quran; na (kujuvywa) ilimu nyingine
anazokuonyeeni. Na mcheni Mwenyezi Mungu na jueni kwamba Mwenyezi Mungu ni
mjuzi wa kila kitu.” (Quran 2:231) “Na wale wanaofishwa (wanaokufa) miongoni mwenu
na kuacha wake; hawa (wake) wangoje (wasiolewe) miezi minne na siku kumi. Na
wanapofikia muda wao (wa kumaliza eda yao hiyo), basi si dhambi juu yenu kwa
yale wanayoyafanyia nafsi zao (hao wanawake) kwa yanayowafiki (kufuata) Sharia.
Na Mwenyezi Mungu anazo habari za yote mnayoyatenda. (Quran 2:234) “Na wale
wanaofishwa (wanaokufa) miongoni mwenu na wakawaacha wake, wawausie (mawarithi
wao) kwa ajili ya wake zao kupata matumizi kwa mwaka mmoja bila ya kutolewa
katika majumba waliyokuwamo ya waume zao.
Ukewenza
Ukewenza
Mitala
ni jambo la zamani sana linalopatikana katika jamii za kibinadamu nyingi na
Biblia haijakemea mitala. Kwa kulinganisha, Agano la Kale na maandiko ya
wanazuoni wa Kiyahudi mara kwa mara yanathibitisha haki ya mitala. Inasemekana
kuwa mfalme Suleimani alikuwa na wake 700 na masuria 300. (1 Wafalme 11:3) Vile
vile, mfalme Daudi, inasemekana alikuwa na wake wengi na masuria pia (2 Samweli
5:13). Agano la Kale lina sheria za kugawa mali za mume na kuwapa watoto wake
kutoka kwa wake mbali mbali. (Kumb. 22:7).
Kizuizi
cha pekee dhidi ya mitala ni kuharamishwa kumtwaa dada wa mkeo awe mke mwenza.
(Walawi 18:18). Talmudi inashauri idadi ya mwisho kuwa ni wake wane 51 na Wayahudi
wa Ulaya waliendelea kufanya mitala hadi karne ya kumi na sita.
Makanisa
ya Kiafrika na Wakristo wa Kiafrika mara nyingi wanawakumbusha wenziwao wa
Ulaya kuwa Kanisa kuharamisha mitala ni mila za utamaduni na sio amri ya sheria
thabiti ya Kikristo. Quran, vile vile imeruhusu ukewenza, lakini sio bila ya
mipaka: “Na kama mkiogopa kutowafanyia uadilifu mayatima (basi ogopeni vile
vile kutowafanyia uadilifu wanawake). Basi oeni mnaowapenda katika wanawake,
(maadamu mtawafanyia insafu) wawili au watatu au wanne tu. Na mkiogopa kuwa hamuwezi
kufanya uadilifu, basi oeni mmoja tu, au (wawekeni masuria) wale ambao mikono
yenu ya kiume imewamiliki. Kafanya hivi ndiko kutapelekea kutofanya jeuri”
(Quran 4:3). Quran kinyume na Biblia, imeweka mipaka ya idadi ya wake hadi
wanne tena chini ya masharti makali ya kuwatendea hao wake kwa usawa na
uadilifu. Isifahamike kuwa Quran inawahimiza waumini wafanye mitala, au kuwa na
mitala ndio ukamilifu. Kwa maneno mengine, Qurani “imesamehe” au “imeruhusu”
mitala, na si zaidi, lakini kwa nini? Kwa nini mitala imeruhusiwa? Jibu ni
lepesi: kuna maeneo na nyakati ambazo zinalazimisha jamii kufanya hivyo, pia
malengo ya kimaadili ya kuwepo kwa mitala. Kama aya ya Quran iliyopo hapo juu
ilivyoonyesha, mada hii ya mitala katika Uislamu haitofahamika peke yake nje ya
shuruti za jamii na kuhusu mayatima na wajane.
Uchunguzi
uliofanywa vijijini Kenya, wanawake 25 katika kila 27 wanapendelea ukewenza
kuliko kuwa mke mmoja tu. Wanawake hao wanahisi kuwa ukewenza ni furaha na
unafaida kama wake wenza watashirikiana na kusaidiana. Uchunguzi uliowahusisha
zaidi ya wanawake elfu 6, wenye umri wa kati ya miaka 15 hadi 59, walio katika
mji wa pili kwa ukubwa nchini Nigeria wameonyesha kuwa asilimia sitini 60% ya
wanawake hao watafurahi kama waume zao wataoa wake wengine. Ni asilimia 23% tu
walioonyesha kukerwa na wazo la ukewenza. Asilimia 76% ya wanawake waliofanyiwa
uchunguzi nchini Kenya walionyesha kukubali mitala (Bergin & Garvey,
1994:108-109). Ukewenza katika jamii nyingi za Kiafrika ni msingi unaoheshimika
kwa kiasi ambacho baadhi ya Makanisa ya Kiporestanti yamekuwa yakiruhusu
mitala. Askofu wa Kanisa la Kianglikana nchini Kenya ametangaza kuwa, “Ingawa
kutokuwa na mitala huenda likawa ni jambo bora kwa kuelezea mapenzi kati ya
mume na mke, Kanisa lazima lizingatie kuwa katika baadhi ya tamaduni mitala ni
jambo linalokubaliwa na jamii na kuwa imani ya kuwa mitala ni kinyume na
Ukristo si ya kufuatwa tena.
Baada ya uchunguzi yakinifu juu ya mitala ya Waafrika, Reverend David Gitari wa Kanisa la Kianglikana amehitimisha kuwa mitala ni bora kufanywa, na ndio Ukristo zaidi kuliko talaka na kuoa tena, ili kuwaonea huruma wake walioachwa na watoto wao.
Tatizo la ujinsia usio na uwiano limekuwa ni tatizo sugu nyakati za vita. Makabila ya Wahindi Wekundu, watu asilia wa Marekani walikuwa wanasumbuliwa kwa kiasi kikubwa na tatizo la ujinsia usio na uwiano baada ya kumalizika vita wakiwa wameshindwa. Wanawake katika makabila hayo, ambao kwa hakika walifurahia hali ya kijamii ya hali ya juu, walikubali mitala kuwa ndio kinga bora zaidi dhidi ya matendo ya mahusiano yasiyo na heshima.
Baada ya uchunguzi yakinifu juu ya mitala ya Waafrika, Reverend David Gitari wa Kanisa la Kianglikana amehitimisha kuwa mitala ni bora kufanywa, na ndio Ukristo zaidi kuliko talaka na kuoa tena, ili kuwaonea huruma wake walioachwa na watoto wao.
Tatizo la ujinsia usio na uwiano limekuwa ni tatizo sugu nyakati za vita. Makabila ya Wahindi Wekundu, watu asilia wa Marekani walikuwa wanasumbuliwa kwa kiasi kikubwa na tatizo la ujinsia usio na uwiano baada ya kumalizika vita wakiwa wameshindwa. Wanawake katika makabila hayo, ambao kwa hakika walifurahia hali ya kijamii ya hali ya juu, walikubali mitala kuwa ndio kinga bora zaidi dhidi ya matendo ya mahusiano yasiyo na heshima.
Ni
jambo la kuvutia kujua kwamba katika mkutano wa kimataifa wa vijana uliofanyika
Munich mwaka 1948 tatizo la ujinsia usio na uwiano nchini Ujerumani
lilijadiliwa. Na ilipodhihirika kwa uwazi kuwa hakuna dawa iliyoafikiwa, baadhi
ya washiriki walipendekeza mitala. Jibu la kwanza la washiriki wa mkutano huo
lilikuwa ni mchanganyiko wa mshtuko na kero. Hata hivyo, baada ya uchunguzi wa
kina juu ya pendekezo hilo, washiriki walikubaliana kuwa jambo hilo lilikuwa
ndio utatuzi wa pekee. Kwa hiyo, mitala ilihitimishwa kuwa ni miongoni mwa
mapendekezo ya mwisho ya mkutano huo.
Ulimwengu leo hii unamiliki silaha nyingi za maangamizi kuliko ilivyokuwa hapo kabla na makanisa ya Ulaya hivi karibuni au baadaye, yatalazimika kukubali mitala kuwa ndio njia pekee. Huonesha nia ya mwanamke mmoja kutokuwa mchoyo kwa mwanamme.
Ulimwengu leo hii unamiliki silaha nyingi za maangamizi kuliko ilivyokuwa hapo kabla na makanisa ya Ulaya hivi karibuni au baadaye, yatalazimika kukubali mitala kuwa ndio njia pekee. Huonesha nia ya mwanamke mmoja kutokuwa mchoyo kwa mwanamme.
Billy
Graham, mwinjilisti maarufu wa Kikristo ameutambua ukweli huo: “Wakristo
hawawezi kuafiki suala la mitala. Kama sasa hivi Wakristo hawawezi kufanya
hivyo, huko ni kujivunja wenyewe. Uislamu umeruhusu mitala kama ni utatuzi wa
matatizo ya kijamii na umeruhusu kiwango maalumu cha uhuru wa kimaumbile ya
kibinadamu lakini hayo yote yakiwa katika mzingo wa sheria kali
zilizotambulishwa. Nchi za Kikristo zinaonyesha maonyesho makubwa ya ndoa za
mke mmoja, lakini kwa hakika zinatekeleza mitala. Hakuna mtu asiye na mwanamke
zaidi ya mkewe, kuna vimada vinavyowekwa katika jamii za Kimagharibi. Kwa hiyo,
Uislamu ni dini ya kuheshimika yenye wema wa kimsingi, na umemruhusu Mwislamu
aoe mke wa pili kama atalazimika, lakini pia umeharamisha vikali mno aina zote
za ndoa za siri na uzinzi unaohusika ili kulinda uaminifu wa kimaadili wa
jamii.”
Biblia,
kwa upande mwingine na wakati mwingine inakimbilia ndoa za mitala za lazima.
Mjane asiye na mtoto lazima aolewe na ndugu wa mumewe, hata kama tayari
ameshaoa (tazama sehemu ya “Matatizo ya Wajane”), bila kujali radhi zake.
(Mwanzo 38:8-10). Ifahamike kuwa katika jamii nyingi za leo hii suala la
kutekeleza mitala ni chache mno kwa kuwa mwanya kati ya idadi ya jinsia mbili
ya kike na ya kiume si mkubwa. Mtu, kwa kujiamini, anaweza kusema kuwa kiwango
cha ndoa za mitala katika ulimwengu wa Kiislamu ni kidogo sana kulinganisha na
kiwango cha ngono za nje ya ndoa katika nchi za Kimagharibi. Kwa maneno mengine,
wanaume katika ulimwengu wa Kiislamu leo hii ni wapenda mke mmoja sana kuliko
wanaume katika nchi za Kimagharibi. Ni jambo la kuzingatia kuwa, katika nchi
zisizo za Kiislamu na za Kiislamu ulimwenguni, leo hii, kuna mitala ya kinyume
cha sheria. Kujitwalia mke wa pili hata kwa radhi za mke wa kwanza, ni uvunjaji
wa sheria. Lakini kwa upande mwingine, kumdanganya mke, bila kujua au kutoa
radhi zake, ni jambo linalokubalika.
Kwa
kurejelea Biblia takatifu, dhana ya ufeministi imejadiliwa na kisha kuibua
harakati baada ya kuwepo kwa mifumo ya ukandamizwaji wa mwanamke kama
inavyoonyeshwa katika vifungu mbalimbali:
1Timotheo
2:11-18 “mwanamke na ajifunze katika utulivu, akitii kwa kila namna na kwa
unyenyekevu. Simpi mwanamke ruhusa ya kufundisha, wala kumtawala mwanaume, bali
awe katika utulivu. Kwa maana Adamu ndiye aliyeumbwa kwanza na Hawa baadaye.
Wala Adamu hakudanganywa, ila mwanamke alidanganywa kabisa akaingia katika hali
ya kukosa…”
1Wakorintho
11:7-10 “kwa maana kweli mwanaume haimpasi kufunika kichwa kwa sababu yeye ni
mfano na utukufu wa Mungu. Lakini mwanamke ni utukufu wa mwanaume. Maana
mwanaume hakutoka katika mwanamke bali mwanamke katika mwanaume. Wala mwanaume
hakuumbwa kwa ajili ya mwanamke bali mwanamke kwa ajili ya mwanaume. Kwa hiyo
imempasa mwanamke awe na dalili ya kumilikiwa kichwani, kwa ajili ya malaika.
1
Wakorintho 14: 34-36”Wanawake na wanyamaze katika Kanisa, maana hawana ruhusa
kunena bali watii kama vile inenavyo torati. Nao wakitaka kujifunza neno
lolote, na wawaulize waume zao wenyewe nyumbani mwao; maana ni aibu wanawake
kunena katika kanisa…”
Walaka
wa kwanza kwa Wakolintho 14:34-35 unasema kuwa: Wanawake na wanyamaze katika
kanisa, maana hawana ruhusa kunena bali watii, kama vile inenavyo torati nayo.
Nao wakitaka kujifunza neno lo lote, na wawaulize waume zao wenyewe nyumbani
mwao; maana ni aibu wanawake kunena katika kanisa. Au je! Neno la Mungu lilitoka kwenu? Au kuwafikia ninyi peke yenu?
Mtu akijiona kuwa ni nabii au mtu wa rohoni, na ayatambue hayo ninayowaandikia,
ya kwamba ni maagizo ya Bwana.
Fundisho
kuu lilikuwa ni kusema kwamba imani pekee inatosha, hakuna haja ya matendo kwa
kuwa ulimwengu wa kiroho haulingani na ulimwengu halisi wa kimwili. Kwamba
Mungu ni roho na mambo yake ni ya rohoni. Kwamba binadamu ana sehemu mbili
(Pyisical & Spiritual) upande wa
spiritual ndiko binadamu hufanana na MUNGU na anapaswa kuamini tu ikatosha.
Upande wa pyisical ni masuala ya kimwili, na hayawezi kulingana na ya kiroho.
Mathayo
15:38 anasema kwamba, “…nao waliokula walikuwa wanaume elfu nne bila wanawake
na watoto”. Hii in maana kwamba katika
mkutano ule walikuwepo watu wake kwa waume lakini wanawake hawakuhesabika.
Harakati za ukombozi wa mwanamke katika
kitabu kitakatifu cha Biblia (ufeministi)
Waamuzi
4:4-10 “Basi Debora, nabii mke, mkewe Lapidothi, ndiye aliyekuwa mwamuzi wa
Israeli wakati ule. Naye alikaa chini ya mtende wa Debora, kati ya Rama na
Betheli katika nchi ya vilima ya Efrahimu; wana wa Israeli wakakwea kwake awaamue…”.
Maneno haya yanamsawiri mwanamke kama my mwenye kutoa maamuzi sahihi katika
jamii yake.
Matendo
ya Mitume 9:36-40 “Na mwanafunzi mmoja alikuwako Yafa, jina lake Tabitha,
tafsiri yake ni Dorkasi (yaani Paa) mwanamke huyu alikuwa amejaa matendo mema
na sadaka alizozitoa…” Hii inaonesha ni kwa kiasi gani mwanamke anasawiriwa
kuwa mtu mwenye matendo safi.
Marko
16:1-12 “Hata sabato ilipokwisha kupita, Mariamu Magdalena na Mariamu mamaye
Yakobo, na Salome walinunua manukato wapate kwenda kumpaka…” Wanawake ni watu
wema na wakarimu kwani huweza kuwa huruma dhidi ya watu wanaopata mateso.
Esta
4:4-15 “Basi wajakazi wa Esta, na wasimamizi wake wa nyumba wakamjia, wakampasha
habari; naye Malkia akahuzunika mno;…” Mwanamke ameitwa malkia ikiwa na maana
ya mtawala. Hivyo mwanamke anaweza kuwa mtawala na akatawala nchi au eneo
fulani kwa mafanikio makubwa.
Luka
10:38-42 “Ikawa katika kuenenda kwao aliingia katika kijiji kimoja; mwanamke
mmoja jina lake Martha akamkaribisha nyumbani kwake. Naye alikuwa na umbu lake
aitwaye Mariamu, aliyeketi miguuni pake Yesu, akisikiliza maneno yake. Lakini
Martha alikuwa akihangaika kwa utumishi mwingi; akamwendea, akasema, Bwana,…”
Rejea
hizi katika Biblia Takatifu zinaonesha ni kwa jinsi gani mwanamke alikwishaanza
harakati za kujikomboa na kuanza kufanya mambo ambayo hayakutegemewa kufanywa
naye mfano unabii, uongozi na utumishi.
Pamoja
na hayo, wanawake ndani ya taasisi mbalimbali mfano kanisani, wanashiriki
katika kuendesha semina na mafundisho mbalimbali mfano Mchungaji Rwakatale
Getruda. Aidha, wamefanikiwa kuanzisha vyama mbalimbali ndani ya taasisi hizo
mfano Dorikasi (chama cha wanawake makanisani) ambacho hujishughulisha na
shughuli mbalimbali za kiuchumi, WAWATA, BETHANIA na Karsimatiki.
Pia
katika uenezaji wa injili kwa njia ya nyimbo, wanawake wanaonekana kuwa mstari
wa mbele mfano Rose muhando, Bahati Bukuku, Christina Shusho na Jennifa Mgendi;
kitu kinachodhihilisha mabadiliko na kujishughulisha kwao katika kutekeleza
majukumu ya kijamii.
Dini ya uislam inatofautiana au
kufanana na dini ya ukristo katika Ufeministi
Maandiko mbalimbali yanasisitiza kuwa fikra hii
inapingana na itikadi na mafundisho ya Uislamu unaomtambua mwanamke na mwanaume
kuwa wanakamilishana ndani ya familia na katika jamii. Itikadi za kifeministi
zinakukosoa misingi ya mrengo huo katika mtazamo wa dini ya Uislamu
ikilinganisha na ukristo.
Pamoja
na kwmba tumeona mjadala mrefu juu ya uthamini wa mwanamke katika dini za
kikristo na uislam, bado mwanamke wa kikristo anayo haki ya kusimama mbele ya
kanisa (waumini) na kuhubiri au kuendesha mafunzo ya biblia kwa watu wote mfano
mchungaji Faith Rugazia, Halice Kabugumila na Getruda Rwakatale. Hii
inadhihirisha harakati za ukombozi kwa wanawake wa kikristo tofauti na ilivyo
kuwa katika Uyahudi. Katika upande wa waislam dhana ya ufeministi bado
haijajidhihirisha kwani mwanamke wa kiislam hawezi kuongoza ibada ya waumini
wote (wake kwa waume).
Katika
ukristo, suala la ufeministi limeibuliwa kwa kuonyesha ukombozi wa kifikra juu
ya ndoa ya mke mmoja tofauti na waislamu ambapo mwanaume anaruhusiwa kuoa
mwanamke zaidi ya mmoja. Hii inaondoa usawa kati ya mwanamke na mwanamme kwa
sababu mwanamke hawezi kuwa na wanaume wawili ila mwanamme anaweza. Lakini pia,
hali ya kuwa na mke mmoja inaashiria uchoyo kwa wanawake waliokwisha olewa
maana takwimu zinaonesha kuwa idadi ya wanawake ni kubwa kuliko wanaume.
Ufeministi
pia unaonekana au unajitokeza kwa wakristo pale ambapo wanawake huondokana na
kasumba za kutochangamana na wanaume (kukaa pamoja katika ibada). Kwa sasa
wanawake hukaa pamoja na wanaume wakibadilishana mawazo. Kwa upande wa dini ya
kiislamu bado wanawake hawaruhusiwi kuchangamana na wanaume (kukaa pamoja
wakati wa ibada) kwani hutenganishwa na ukuta kati yao na hivyo kutopata fursa
ya kubadilishana mawazo kati yao na wanaume.
Hapo
kale mwanamke alikuwa haruhusiwi kwenda ibadani kama yupo katika hedhi kwani
aliitwa najisi. Lakini baada ya kugundulika kuwa ni badiliko la kawaida katika
mwili wa mwanamke, sasa mwanamke wa kikristo anashiriki ibada. Harakati hizi
bado hazijamfikia mwanamke wa kiislamu kwani yeye akiwa katika hedhi bado
haruhusiwi kufunga na kufanya ibada msikitini.
Ufeministi
kwa wanawake wa kikristo pia umeonekana pale ambapo wanakwenda makaburini kwa
ajili ya kumzika marehemu jambo ambalo ni tofauti kwa mwanamke wa kiislam. Wao
hawaendi makaburini na hubakia nyumbani kana kwamba hawawezi kuweka udongo
kaburini. Hili jambo linaonekana kwenda kinyume na usawa wa wanawake kwa
wanaume. Fikilia kama mtu amefariki mikonooni mwa wanawake, je hatazikwa?
Suala
la mfanano juu ya dhana ya ufeministi kati ya wakristo na waislam haliko wazi
kutokana na kutokuwepo kwa harakati za kumkomboa mwanamke wa kiislamu ukiliinganisha
ukristo baada ya ujio wa Kristo na kuachana na dini za kiyahudi zilizojikita
katika sheria (torati). Hii ni kutokana na kuiamini Quran tukufu kwamba
yaliyosemwa juu ya mwanamke yanapaswa kubaki vilevile kwani ni agizo la Mungu
na sio ukandamizaji. Bado dini ya uislam
inalinganisha ukristo wakati wa sheria za Kiyahudi na si baada ya ujio wa
Kristo.
Hivyo
basi, kwa kuirejelea biblia, ufeministi umekuwepo ili kumkomboa mwanamke au
kumfanya aweze kushika nyadhifa mbalimbali za uongozi mfano ushemasi na
uchungaji, kuendesha semina na mihadhara mbalimbali, kuketi pamoja na wanaume ili
kubadilishana mawazo, kushiriki shughuli za uchumi na ujenzi wa kanisa na
kuilea jamii katika maadili yapasayo.
Nadharia ya Ufeministi katika Fasihi
ya Kiswahili
Wamitila
(2006:160-161) na Ntarangwi (2004:52-56) wamebainisha ukandamizaji mbalimbali na
harakati za ukombozi (Ufeministi) katika maisha ya jamii ya kiafrika kupitia
katika kazi mbalimbali za kifasihi. Ni kweli kwamba kuna baadhi ya harakati za
ufeministi zinakinzana na maisha halisi ya mwanamke wa Kiafrika lakini baadhi
ya harakati hizo zanasawiri maisha halisi ya mwanamke wa kiafrika kama
ifuatavyo:
Katika
kubainisha umuhimu wa mwanamke kutokana na mwanamke kukulia katika jamii zenye
mfumodume Ufeministi Ufeministi umesawiliwa. Awali umuhimu wa mwanamke
haukuonekana, ndiyo maana ikaanzishwa nadharia ya ufeministi ambayo yenyewe
iligundua umuhimu wa mwanamke katika jamii. Umuhimu wake upo katika nyanja zote
za kiuchumi, kijamii, kisiasa na kiutamaduni. Mfano, katika nyanja ya kisiasa
mwanamke anaweza kuwa kiongozi bora na mwenye ushauri. Hili linajidhihirisha
katika riwaya ya Barua
Ndefu Kama Hii iliyoandikwa
na Mariama Bâ (1994). Mwandishi anathibitisha hili anaposema:
“Tunayo karibu miaka ishirini ya uhuru! Lini
tutampata mwanamke wa kwanza awe waziri atakaye husishwa na maamuzi
yatakayoongoza nchi yetu huko tuendako? Kumbe nguvu walizonazo wakina mama,
uwezo wao wa kupambana, na kujihusisha kwao bila kutegemea kupata faida yoyote
ni mambo ambayo hayahitaji tena kuthibitishwa. Wanawake wamewainua wanaume
wengi kwenye ngazi za juu” (uk.82)
Mwanamke ameonekana kama mlezi wa familia katika jamii;
Mfano, Ramatulayi katika riwaya ya Mariama Ba (1994) anailea familia yake kwani
ameweza kulipa bili ya maji, umeme bila hata kumtegemea mwanaume. Mfano,
mwandishi anasema:
“Licha ya
mzigo niliokuwa nao tangu zamani, nikaubeba na ule uliokuwa wa Modu. Ununuzi wa
vyakula muhimu ulinishughulisha kila mwisho wa mwezi. Nilihakikisha kwamba sikuwa na upungufu wa nyanya au mafuta, viazi
mviringo na vitunguu wakati ambapo vyakula hivi viliadimika sokoni… Nilikuwa
mwangalifu kuzilipa bili za maji na umeme pindi zilipofika.” (uk.69)
Mtembei (2012) akimnukuu Angelica Baschiera (2003)
anadai kuwa, Penina Muhando ni mmoja wa waandishi mashuhuri wanawake wanaojulikana
nchini mwake na kimataifa. Kutokana na uandishi wake ameweza kupata tuzo ya
kimataifa ya ‘‘Africa Education
Journalism.’’Alikuwa mmoja wa waanzilishi wa mkabala wa Thieta kwa
maendeleo katika Afrika ambamo ubunifu wa sanaa za maonesho hutumiwa na
wananchi katika jamii zao kujiletea maendeleo yakiwamo ya kielimu.
Kawiche
(2000) anasema kuwa, Penina Muhando ametumia ufeministi kumchora mwanamke.
Amempa mwanamke nafasi ya kipekee. Pia, anatetea maslahi ya wanawake katika
kazi zake za fasihi, kupitia wahusika aliowachagua kufikisha ujumbe. Anatambua
umuhimu wa wanawake katika jamii. Pia, anadai kuwa, mwanamke kwenye suala la
uongozi anaweza, ingawa anaweza kukandamizwa katika jamii za ulimwengu kwa
sababu ni mwanamke na pia, mfanyakazi wa nyumbani, kama ilivyojitokeza katika
tamthiliya zake za Hatia, Heshima Yangu na Nguzo Mama na mbinu
zilizotumika kusawili. Watafiti mbalimbali wamehakiki tamthiliya za Penina
Muhando, wengi wao wameelezea fani na maudhui na nafasi ya mwanamke katika
jamii.
Kuondoa utegemezi wa wanawake kwa wanaume; lengo
hili la ufeministi linakinzana na maisha halisi ya mwanamke wa Kiafrika. Kwa
kuwa mwanamke wa Kiafrika anaonekana hana umuhimu katika jamii, pia anaonekana
kuwa dhaifu ambaye hawezi kuiendesha familia yake bila msaada wa mwanaume hii
ni kutokana na jamii nyingi kuendeshwa na mfumodume. Kihistoria wanawake wamekuwa ni tegemezi na wasaidizi wa
wanaume, ni kweli kihistoria wanawake wamekuwa wategemezi na wasaidizi wa
wanaume. Mfano katika tamthiliya ya Nguzo Mama iliyoandikwa na
Penina Muhando (2007) tunaona mhusika BI MOJA alivyokuwa akimtegemea mume wake
na kutaka anunuliwe kanga. Mwandishi anasema:
“BI MOJA: (kwa Shaabani): Kama ulijua kufika sasa hivi
nipe hela ya kanga bwana meli meli hii hainikosi leo utanipa hela hizo kanga
nikakate. Mwezi wa tatu huu kanga sizijui.
Shaabani: Nimekuambia mimi hela sina. Sasa
unataka nikaibe?”(uk.31-32)
Ni kweli kwamba mwanamke wa kiafrika amekuwa
tegemezi katika jamii, kwani humtegemea mwanaume katika mambo mbalimbali ya
kifamilia. Kwa mfano kutafuta au kununua mahitaji ya nyumbani kama vile
chakula, mavazi yake na watoto wake au kulea watoto wake.
Lakini kupitia katika utendaji wa nadharia
hii, wanawake wameweza kuhamasishwa katika Kujitegemea kufanya kazi na
kujipatia pato halali.
Kuondoa ukandamizaji wa mwanamke kutokana na
pingu za kiutamaduni, kijamii, kidini, kisiasa na kiuchumi. Jamii nyingi za
Kiafrika zimejengeka katika mfumodume, hivyo basi jamii zinamkandamiza mwanamke
kutokana na pingu hizo. Katika kulithibitisha hili waandishi wa kazi za fasihi
nao hawakuwa nyuma kulizungumzia katika kazi zao na lengo ni kuondoa mfumodume
uliojengeka muda mrefu katika jamii. Kwa upande wa
kiutamaduni mwanamke ameonekana kukandamizwa kwa kuonekana hana mamlaka hata ya
kurithi mali za mumewe au zake mwenyewe, badala yake hata akifiwa na mumuwe
anapigwa, anafukuzwa na kudhalilishwa. Penina Muhando anayathibitisha haya
katika tamthiliya yake ya Nguzo Mama kwa kumtumia BI SABA pale
anaposema:
“Akalia
Bi Saba tena akalia
Hana
wa kumsaidia
Mumewe
kafa nduguze wakaja juu
Pesa
wamechukua senti tano haikubaki
Vyombo na nguo zote
wakagawana
Roho
ilimpasuka Bi Saba kuwaona hao ndugu
Walivyogombania
mali wasiyoichuma…
Sasa juu ya yote haya
wamerudi kufagia
Hata ufagio wamebeba
Na
lawama kumtupia eti pesa kazificha.” (uk.39)
Kuhamasisha mwanamke kujishughulisha na kazi
mbalimbali za kujiletea maendeleo yake binafsi. Kwa kuwa mwanamke amekuwa
anarudishwa nyuma kwa kukandamizwa na mwanaume basi nadharia hii inampa nguvu
ya kuendeleza na mapambano yake. Penina Muhando anayathibitisha haya kwa
kumtumia BI PILI ambaye alikuwa anapika pombe ili kujikwamua katika hali ngumu
ya maisha lakini mumewe SUDI alizichukua hela zote alizokuwa alizozipata. Kwa
mfano, mwandishi anasema:
“BI
MSIMULIZI: Upishi wa pombe balaa ulimzushia
Visa
na mikasa Bi pili havikumuishia
Pesa
alizipata kutokana na hiyo pombe
Lakini
visa vya pombe hiyo pesa hazikufidia”
SUDI: (kwa
Bi Pili) Nani kalewa? Umeninywesha wewe?
Wee!hawara
zako ndiyo wamekutia jeuri unaninyima pesa.
Toa
pesa sasa hivi (Anampiga) Bi Pili anakimbia huku akilia.” (uk.16)
Vilevile nadharia hii inaondoa mila potofu
mfano mwanamke alikuwa anakandamizwa kwa kulazimishwa kurithiwa na kaka au
ndugu wa mume pindi anapofiwa na mumewe. Mwandishi analithibitisha hili katika
riwaya ya Barua Ndefu Kama Hii pale anaposema:
“Tamsiri,
zitapike hizo ndoto zako za kutaka kuniposa.
Umeshakaa
nazo kwa siku arobaini. Kamwe sitokuwa mkeo.”(uk.81)
Mwandishi anamchora mwanamke akimweleza mwanamme
kuacha ndoto zake za kutaka kumposa mjane. Mwanamke mjane anaonesha kuwa imara
katika maamuzi yake na kwenda kinyume na mila potofu.
Kwa upande wa kisiasa, mwanamke amekuwa
akikandamizwa kwa kuonekana hawezi kuwa kiongozi bora wa kuiongoza nchi ndio
maana hata nafasi za wanawake zilikuwa chache huko bungeni. Katika riwaya
ya Barua Ndefu Kama Hii iliyoandikwa na Mariama Bâ mwandishi
anayadhihirisha haya kwa kumtumia Ramatoulayi ambaye akilalamika kuhusu
ukandamizwaji wa wanawake huko bungeni pale anaposema:
“Wanawake
wanne, Dauda, wanne miongoni mwa wabunge mia moja uwiano gani huu wa kimzaha!
Wala hakuna uwakilishaji wa kimkoa” (uk.81)
Wanawake wanaonekana kushika nyadhifa
mbalimbali za uongozi lakin bado hawakubaliani na uwiano uliopo kati ya
wanawake na wanaume. Mwandishi anaonyesha wanawake kuendeleza mapambano dhidi
ya kushika nyadhifa mbalimbali ili kuleta uwiano wa katika kutoa maamuzi juu ya
maendeleo ya nchi yao.
Kwa upande wa kijamii, mwanamke amekuwa
akikandamizwa kwa kupigwa na mumewe bila sababu zozote za msingi. Hili
linajidhihirisha katika riwaya ya Rosa Mistika iliyoandikwa na
Euphrase Kezilahabi (1988) kwa kumtumia mhusika Zakaria ambaye alikuwa anampiga
mkewe bila sababu. Mwandishi anasema:
“Regina
tangu aolewe hakuwa na raha! Alikuwa akisumbuliwa na kuteswa na mumewe kwa kosa
lisilokuwa lake. Katika kijiji chote cha Namagondo hapakuwa na mwanamke
aliyekuwa akipigwa karibu kila juma kama Regina. Wanawake wengi kijijini
walijiuliza kwa nini hakutaka kumuacha bwana wake. wengine walimuonea huruma,
wengi lakini walimuona mjinga.” (uk.3)
Pi, mwanamke alikuwa anakandamizwa kwa
kuonekana kuwa yeye ndiye mwenye majukumu ya malezi, kwa hiyo hata watoto
wakiharibika anayelaumiwa ni mwanamke. Euphrase Kezilahabi analithibitisha hilo
pale anaposema:
“Lete
hiyo barua iko wapi? Pamoja na shilingi ulizopewa unafikiri sisi hapa maskini.
Rosa alipigwa tena na tena. Makofi yalikwenda mfululizo hata damu zikamtoka
puani na mdomoni. Baba nihurumie sitarudia tena… Zakaria hakujali alichukua
fimbo na kuongozana na bintiye mpaka chumba cha watoto hali akinguluma lazima
unioneshe barua hiyo unataka kuniletea umalaya wa mama yako hapa.” (Uk.7)
Vilevile, mtoto wa kike alikuwa anaonekana
hana thamani katika jamii, na watoto wa kiume ndio waliopewa kipaumbele.
Euphrase Kezilahabi anathibitisha haya katika riwaya ya Rosa
Mistika kwa kumtumia Zakaria ambaye kabla ya kumpata mtoto wa kiume
alikuwa anamnyanyasa sana mke wake lakini baada ya kujifungua mtoto wa kiume
manyanyaso yaliisha na alimpenda sana mkewe. Mwandishi anasema:
“Zakaria
alirudi nyumbani siku hiyo. Alikuwa amekwisha pata habari hizo njiani. Alimbeba
mtoto. Alimpa pongezi mke wake. Regina sasa mji huu umekuwa wako. Asante Regina
alijibu akitabasamu, alijiona anauwezo wa kuzungumza.”(uk.24)
Pamoja na hayo, lengo hili linakinzana na maisha halisi ya mwanamke wa Kiafrika,
kwani mwanamke hakutakiwa kurithi mali yoyote pindi wazazi wake wanapofariki au
mumewe anapofariki. Pia mwanamke kushindwa kupewa nafasi ya kutoa maamuzi
yoyote katika masuala ya kiukoo. Kwa upande wa dini mwanamke anakandamizwa na
kuonekana dhaifu hivyo kutokuwa na nafasi ya kuongoza waamini. Mfano, dini ya
Kiislamu na baadhi ya madhehebu ya Kikristo.
Wanawake wanafanya juhudi za kuzitambua na
kuzibainisha dhamira kuu katika kazi zilizoandikwa na wanawake. Dhamira kuu ni
dhamira inayomsukuma mwandishi katika kuandika kazi ya fasihi. Baadhi ya
waandishi wanawake wameonesha dhamira kuu katika kazi zao ni kama:
Nguzo Mama iliyoandikwa na Penina Muhando (2007)
imebeba dhamira kuu ambayo ni ukombozi wa mwanamke. Ukombozi huo upo katika
nyanja mbalimbali kama vile kijamii, kiutamaduni, kiuchumi na kisiasa. Mfano,
mwandishi ameonesha wanawake wanavyojishughulisha katika kuinua uchumi wao,
kwani walikuwa wakiuza vitambaa na kupika pombe. Mwandishi anathibitisha haya kwa
kusema:
“BI
TANO: Yaani mnasema mimi mvivu siyo nimezunguka mji mzima na zigo hilo halafu
mnaniambia mimi mvivu. Nawaambia watu hawataki kununua au mnataka niwagawie
bure.”
BI
NANE: Lakini kwa nini wakatae kununua hivi, mbona vile vya mwanzo walivinunua? (uk.16).
Vilevile, Katika riwaya ya Barua Ndefu
Kama Hii iliyoandikwa na Mariama Bâ (1994) suala la ukombozi wa
mwanamke limejitokeza kama dhamira kuu. Ukombozi huu umejikita katika nyanja za
kisiasa, kiutamaduni, kijamii na kiuchumi.
Mfano, katika nyanja ya kijamii, mwandishi
ameonesha jinsi ya kumkomboa mwanamke kielimu, pale anaposema:
“…Shangazi
Nabu anampeleka Nabu mdogo katika shule ya Kifaransa huko. Huko Nabu alijifunza
aina mbalimbali za mapishi, matumizi ya pasi na zana za kutumia na kumenyea...”
(uk.39)
Lengo hili linakinzana na maisha halisi ya
mwanamke wa Kiafrika, kwa kuwa tangu mwanzo wanawake walikuwa hawaruhusiwi kuwa
viongozi, badala yake wanaume ndio waliochukuwa jukumu hilo la uongozi katika
jamii. Pia, wanawake hawakuruhusiwa kupata elimu wakitegemezwa katika majukumu
ya nyumbani na kuandaliwa kwenda kuolewa na kuja kuwa walezi wa familia.
Kuichunguza historia ya kifasihi ya jadi ya
kike na kuwamulika waandishi wa kike waliotambua hali za wanawake na ambao
wanaweza kuchukuliwa kama vielelezo kwa wasomaji wao. Hapo awali kazi
mbalimbali za kifasihi za jadi za kike zilielezwa na waandishi wa kiume. Lakini
nadharia hii imemulika waandishi wa kike wanaotambua hali mbalimbali na
wameamua kuandika kazi mbalimbali ambazo zinaelezea matatizo ya wanawake.
Mfano, katika tamthiliya ya Nguzo Mama mwandishi anaelezea
jinsi wanawake wanavyonyanyaswa na kuachiwa majukumu ya kulea familia,
kuchukuliwa mali zilizoachwa na waume zao baada ya kufariki. Mfano, mwandishi
anasema:
“…Haa!
Shemeji mmerudi kuchukua hata kitanda! Hata sufuria! Nitalala wapi na nitapikia
wapi jamani!” (uk.39)
SUDI: Haya nipe pesa
ulizokwisha kupata.
BI PILI: Hee! Kwa nini
nikupe?
SUDI:
Leta pesa upesi kabla sijakukong’ota.” (uk.13)
Mariama Bâ naye ni kielelezo kwani ameelezea
matatizo mbalimbali yanayowakumba wanawake na namna wanavyokabiliana na
matatizo hayo. Mfano mwandishi anasema:
“…
Ramatulayi, Acha nisikilize mimi zaidi; Redio ya Kankan ilinifahamisha kwamba
ulikataa kuolewa na Tamsiri. Ni kweli? Ndio.” (uk.87)
Mwandishi anaonesha jinsi mhusika
Ramatulayi alivyojitambua na kukataa kurithiwa na Tamsiri, pia anamkataa Dauda
ambaye alitaka kumrithi baada ya kufiwa na mume wake.
Kupitia lengo hili tunaona wanaufeministi
wameongelea kuhusu wanawake tu ambao ni vielelezo katika kazi za fasihi, lakini
wapo wanaume ambao wamezungumzia masuala mbalimbali yanayowahusu wanawake.
Mfano, Shaaban Robert aliyeandika Wasifu wa Siti Binti Saad.
Kudhihirisha kuwa kuna sifa fulani za kike na
uzoefu fulani wa kike katika uwazaji, hisia, kutathmini, kujiangalia na
kuuangalia ulimwengu wao wa nje. Uzoefu fulani wa kike unajitokeza katika
uwazaji na jinsi wanavyousawiri uhalisi. Kazi ambazo zinamsawiri mwanamke kwa
njia chanya, mfano ni riwaya ya Kiwasifu ya Shaaban RobertWasifu wa Siti Binti
Saad. Kuna mashairi kadhaa aliyoyatunga mwandishi ambayo
yanaendeleza suala hili la uchanya wa wanawake katika jamii. Mfano wa usawiri
wa wahusika linathibitishwa pale mwandishi anaposema:
“Siti
binti Saad,
Ulikuwa mtu lini,
Ulitoka shamba,
Na kaniki mbili chini,
Kama si sauti,
Ungekula nini?” (uk.22)
Hisia; mfano, katika riwaya ya Barua
Ndefu Kama Hii kupitia mhusika Daba alivyomwambia mama yake kuhusu
Benetuu. Mwandishi anasema:
“Hasira
ya Daba iliongezeka zaidi jinsi alivyozidi kuichambua hali ilivyokuwa. “Mama!
Vunja ndoa yako! Achana naye mtu huyu hajatuheshimu, si wewe wala si mimi…
sitaki kukuona unagombania mwanaume na mwanamke mwenye umri sawa na mimi.” (uk.52)
Mwanamke
Kama Kiongozi Mwenye Maamuzi ya Sheria
Kupitia
katika kazi ya Penina Mhando, tunagundua kuwa, mwandishi amemsawiri mwanamke
kama kiongozi ambaye anajiamulia mambo yake mwenyewe. Ilielezwa katika
majadiliano ya vikundi kuwa mfano mzuri unaojitokeza katika kitabu cha
tamthiliya ya Nguzo mama ni pale
Mwenyekiti wa Kamati ya Ushauri anapoamua kesi aliyoisikiliza kwa upande wa
mtoa mashtaka tu wakati mshitakiwa hakuwepo. Bi Nane alihukumiwa kwa kosa la
kuanzisha kikundi cha kupinga juhudi za Wanapatata za kuinua Nguzo Mama wakati si kweli. Lakini kwa
kuwa Mwenyekiti hakutaka kumsikiliza Bi. Nane.
Mwenyekiti anatoa uamuzi wa kumwambia Bi. Nane avunje kikundi chake kwa
kuwa hakikupata kibali cha ofisi ya mshauri na uamuzi ambao unamshangaza Bi.
Nane. Mwandishi anasema,
Bi. Simulizi: Bi. Nane akawaza
Kumbe kazi hii ya uongozi au
Uenyekiti
Inampa mtu uwezo wa kufanya
Mambo kinyume cha kawaida
Vipi mtu akubali kutoa ushauri
Kutumia vitisho
Kufuatia maelezo ya mshitaki peke
yake
Tena yaloyoelezwa wakati mshitakiwa
hakuwepo?
Vipi mwenyekiti bila kamati
Akatoa ushauri katika mashtaka? (uk.
22)
Nukuu hizi zinaonyesha jinsi mwanamke alivyochorwa
kama kiongozi mwenye kufuata sera ya udikteta katika jamii. U-dikteta wa
mwanamke unatokana na kutokujiamini kama kiongozi hivyo huamua kufuata mbinu ya
udikteta ili kuepuka changamoto za wale anaowaongoza.
Kupitia
tamthiliya ya Nguzo Mama tunagundua kuwa, mwanamke amechorwa kama kiongozi
ambaye anafuata sheria na kanuni, ingawa wananchi wa Patata wanamuona kuwa,ni
mkiuka maadili na sheria za uongozi. Kwa mfano, mwenyekiti alichorwa akitumia
nafasi yake ya uongozi kukiuka sheria. Mwandishi anaeleza,
Bi. Simulizi: Sheria hii Bi. Nane hajapata kusikia
Miaka kumi kazi kafanya
Mikutano kwa mamia kazini imefanyika
Na mwenyewe Bi. Nane Katibu hata
Mwenyekiti kashakuwa hajawahi kusikia mikutano ya kikazi kwanza kupata kibali
….. kumbe wakubwa wakiwania vibaya
kukuangusha
Mbinu zote watatumia madaraka
watachukua hata yale wasiyopewa (uk. 22-23)
Mwandishi wa tamthiliya hii
amemsawiri mwanamke kwa upande hasi kwani anaonesha jinsi gani wanawake wanavyotumia
vibaya nafasi za uongozi wanazozipata. Hivyo, si kila mwanamke au mwanamume
anaweza kutumia vizuri nafasi yake katika uongozi.
Kukuza na Kuendeleza Hisia za Umoja
wa Wanawake kama Kundi Linalodhulumiwa.
Kwa kuzingatia mtazamo kike mhusika
Natala katika tamthiliya ya “Natala” ya Kithaka Mberia amesawiriwa kupitia katika tamthilia ya Natala ambapo tunamuona
mhusika Gane akimtia moyo Natala kwa kumuunga mkono katika harakati za kutetea
haki zake (uk 24) Gane anasema
Gane: Usivunjike moyo Natala mapenzi yako imara moyo wako wa
kazi na nidhamu yako thabiti ni
baraka kubwa.
Baraka hizi zitakuwa jahazi la kuwafikisha watoto wako
waendako, naamini hawataachwa nyuma na rika lao.
Natala:
Ahsante kwa maneno yako ya kutia moyo.
Pia tunawaona wahusika Natala na Gane ni wanawake wanaopambana ili kuondoa mila na desturi potofu
zilizopitwa na wakati, dhana hii
imejitokeza pale Natala alipokataliwa kupewa
mwili wa marehemu mume wake na
alipotaka kunyanganywa hati ya shamba.
Hivyo
basi hata katika jamii za sasa wapo wanawake wanaoshirikiana katika kuondoa
mila na desturi potofu zilizo pitwa na wakati zinazowakandamiza wanawake.
Lengo hili la wanaufeministi linaendana na
hali halisi ya wanawake wa Kiafrika, kwa kuwa mawazo ya mwanamke jinsi anavyojiwazia
yeye mwenyewe au kuwawazia wanawake wenzake hutofautiana. Vilevile, hisia za
mwanamke zinaweza kudhihirika katika maandishi na kuonesha jinsi wanavyowaza
katika hali ya kawaida.
Ukweli ni kuwa msisitizo mkubwa kupita kiasi wa
mfumo wa kiliberali juu ya mitazamo ya humanism, uhuru wa mtu binafsi, ubinafsi
na kadhalika vimesambaratisha msingi wa maisha ya kifamilia na kijamii katika
nchi za Magharibi. Vilevile msimamo wa kupinga tofauti za kimaumbile kati ya
wanaume na wanawake na kuamini usawa kamili baina ya wawili hao katika nyanja
za kijamii, uliufanya mlengo wa mafeministi wa kiliberali ukabiliwe na
mikinzano mikubwa. Ni vyema kukumbusha hapa kuwa usawa katika fursa na matunda
yake una maana ya kuwa sawa nyanja zote za ushindani baina ya wanaume na
wanawake; wakati huo vipi wanawake ambao wana mchango makhsusi katika uzazi wa
wanadamu (Reproduction) na ni mwenye nguvu dhaifu zaidi za kimwili
wakilinganishwa na mwanaume hususan katika kipindi cha ujauzito, wataweza vipi
kushindana sawa na mwanaume? Kama atamualika mgeni nyumbani kwake
na kumlisha, atakuwa anamuibia mumewe…” (san. 71a, & Git.Ra).
Yapo mambo kadha wa kadha yanayojitokeza na ambayo
kwayo huwa ni changamoto kwa mwanamke kuendeleza mapambano yake dhidi ya
minyororo kaandamizi. Utafiti huu uligundua kuwa changamoto ambazo zinawakabili
wanawake ni pamoja na; uvivu, usariti, wivu, kutokupendana, ukosefu wa elimu,
umaskini, kubaguliwa, kutoaminiwa ndani ya jamii.
Usaliti
Kwa mujibu wa TUKI (2004) usaliti ni kutoa siri za
nchi kwa adui wa nchi hiyo kwa lengo la kuihujumu; toa mipango ya siri ya
wenzako kwa watu wengine ili wenzako wakamatwe, fitini. Utafiti huu uligundua
kuwa suala la usaliti ni kikwazo kikubwa katika uongozi kwa wanawake. Usaliti
unaonekana kwa wanawake wenyewe kwa wenyewe ambao wanaonekana wanasalitiana.
Usaliti unafanya suala zima la uongozi kuwa gumu na hata ugumu katika
kujikomboa kuondokana na ukandamizwaji unaofanywa na wanaume. Lakini pia
wanawake wanaonekana kuwasaliti waume zao na kuwaingiza katika hatari (tazama
Samson alivyosalitiwa na Mkewe Delila).
Uvivu
Uliokithiri
Neno uvivu lina maana ya hali ya kutotaka kufanya
kazi au hali ya ulegevu katika kufanya kazi (TUKI, 2004). Katika kazi hii
iligundulika kuwa, viongozi wa Patata (wanwake) hawapendi kufanya kazi ya
kuletea maendeleo ya Taifa lao. Wanapanga mambo yasiyotekelezeka na kushindwa
kuyafanyia kazi kwa wakati kulingana na malengo yao
Ukosefu
wa Elimu Miongoni mwa Wanawake
Kwa mujibu wa TUKI (2004) neno elimu lina maana ya
mfumo wa mafunzo yanayopatikana shuleni, vyuoni, maishani. Katika utafiti huu
tuligundua kuwa, tatizo la elimu ni tatizo kubwa ambalo linawakabili. Wanawake
ni kundi ambalo limeachwa nyuma katika masuala ya elimu hivyo basi, kukosekana
kwa elimu kunawafanya wanawake washindwe kushika nafasi za uongozi hasa uongozi
wa juu. Mwandishi anaonesha jinsi ukosefu wa elimu unavyosababisha viongozi
kutokuwa makini.
Kupenda
Starehe
Kwa mujibu wa kamusi ya TUKI (2004) neno starehe
lina maana ya hali ya kutokuweko na shida au usumbufu, burudani; hali ya kuweko
mambo ya anasa au furaha; burudani. Mwanamke anaonekana kupenda kufanya starehe
kuliko kufanya kazi. Bi tatu anaona Nguzo Mama haina faida kwake.Mume na
starehe ndiyo vitu anavyovipenda.Hivyo anawasusia wenzake kwa kutimkia kwenye
Volvo lililomfuata na kuelekea kwenye sherehe.
……Jamani mie naondoka
mnaiona Volvo imenifuata mie….tunakwenda. Kwenye pati na mume wangu leo saa
moja. Lazima nipalilie unga kwa baba watoto wangu ati. Nitakula nini… (Uk.41)
Mfano huo unaonyesha jinsi ambavyo wanawake
wanavyopenda starehe na kwa kuwa tegemezi wa wanaume ambao huonekana ndiyo
wenye haki ya kuwapa starehe wanawake.
Hii yote ni mifumo dume, ambayo wanawake wanaona hawawezi kufanya kitu
pasipo kumtegemea mwanaume.
Umasikini
wa Wanawake
Maskini ni mtu asiyekuwa na pato la kutosha;
fukara, dhalili. Katika utafiti huu iligundulika kuwa suala la umaskini ni
changamoto kubwa katika uongozi kwa wanawake. Umaskini humfanya mtu kukosa
elimu, kuhangaika ili ajikwamue na umaskini kuna mfanya apoteze muda mwingi
katika hilo na kusahahu majukumu yake kama kiongozi. Katika tamthiliya ya Nguzo Mama mwandishi amelionyesha hili
kwa kusema wanawake wa Patata wanalia tabu, Bi tano shida zinamwandama. Watoto
wake wanapata taabu.
Malezi
na Mafundisho Mbalimbali hasa ya ki-mila na ki-dini
Malezi lina maana ya njia za ukuzaji wa mtoto kwa
kutarajia kufuata tabia na mwenendo unaostahili. Utafiti huu ulibaini kuwa,
Mwanamke amejengwa na kuaminishwa na mfumo wa jamii kuwa kazi yake kubwa ni
kulea familia na kukaa nyumbani.
Njia
za Kutatua Changamoto Zinazowakabili Wanawake
Njia zianzofaa katika kutatua changamoto ambazo
zimebainishwa kutatiza mchakato wa wanawake kujikomboa zinapendekewa ili zifanyiwe
kazi kupitia katika taasisi mbalimbali za kijamii kama vile dini, kiuchumi,
kisiasa na kijamii huku mila na desturi zikitazamwa kwa ukaribu zaidi.
Elimu,
Usawa wa kijinsia
na Ujasiliamali
Mabadiliko yanatakiwa kwa mwanamke kwa kufundishwa
elimu ya kijinsia ili waweze kutambua haki zao. Shafi (1999) anaitaka jamii
kukubaliana na mabadiliko yanayofanywa na wanawake. Wanatakiwa wajione wao wote
wako sawa ili kuondoa kasumba ya kuamini kuwa, wanaume wako juu, zaidi ya
wanawake. Wanawake na wanaume wanatakiwa
kuelemishwa kuhusu haki za binadamu. Watu wote ni sawa ili kuondoa vikwazo na
vipingamizi wanavyopata wanawake katika harakati zao. Wanawake wapewe elimu ya
ujasiliamali ili waweze kujitegemea wenyewe pasipo kumtegemea mwanaume. Mila
kandamizi ziangaliwe na jamii ichukue nafasi yake katika kuendana na mila
stahiki kutokana na maendeleo ya teknolojia. Taasisi za kidini ziboreshe Mfumo
wa utoaji huduma na haki sawa kwa watu wote hasa kwa wanawake.
Hitimisho
Kwa kuwa dini ni sehemu ya jamii na wanajamii ndio
waumini wa dini hizo, basi mikakati madhubuti iwepo ili kuwafanya wanawake
wajiskie huru katika suala zima la kuitumikia jamii. Uhalisia wa maisha ya
mwafrika umeonekana kupitia katika kazi mbalimbali za kifasihi zikieleza
uhalisia wa maisha yao. Kazi mbalimbali za fasihi hazikuwa mbali na Vitabu
vitakatifu katika kumsawiri mwanamke kama kiumbe mwenye dhambi, dhaifu, maskini
na mwenye kumtegemea mwanamme katika kutatua matatizo yake.
Hata hivyo, tumeona juhudi mbalimbali za wanawake
katika Biblia wakiwa tayari wameshika nyadhifa mbalimbali na wakilitumikia
kanisa kwa nguvu. Pia katika jamii ya kiafrika wanawake wameonekana wakiwa
msitari wa mbele katika kutoa haki, kuonesha upendo, kuongoza vizuri na kutunza
familia. Wito wangu ni kwa wanaume kuwaunga mkono wanawake katika mapambano yao
ili hatimaye sote kwa pamoja tushilikiane katika kuleta maendeleo kwa kuwa
“umoja ni nguvu…”
MAREJELEO:
Ba,
M. (1994). Barua Ndefu Kama Hii. Tafsiri.Mkuki
na Nyota Publishers
Beltsville, M. D. (1990). Elsayyed Sabiq, Figh al Sunnah; Darul Fatah Lile`lam Al-Arabi, 11th
edition, vol. 2, Abdel-Haleem Abu Shuqqa, Tahreer al Mar`aa fi Asr al
Rasala Kuwait: Dar al Qalam.
Gabriel, G. (2015). Ufeministi,
itikadi na misingi yake. Mwanza:
Serengeti Publishers
Irib, World Service (2014). Matatizo ya Wanawake katika Ulimwengu wa Magharib. http://www.kiswahili.irib.ir/38823 .
James A. B., (1987). Law, Sex and Christian Society in Medieval Europe. Chicago:
University of Chicago Press.
Jeffrey H. T. (1990). Adultery,” Encyclopaedia Judaica, Vol. 2, col. 313 and Standing
Again at Sinai: Judaism from a Feminist Perspective. New York: Harper & Row
Publishers.
Jeffrey,
L. (1994). Struggling to Surrender, Cairo: Amana Publications
Malenya, M. M. (2012), Matumizi ya Lugha katika Fasihi
Simulizi. Mwanza: Inland Press.
Mbunda, M. (1990). Usiku
Utakapokwisha. Dar es Salaam University Press, University of Dar es Salaam.
Metuchen, N. J. (1976). Memories of an Orthodox youth” in Susannah
Haschel ed. On being a Jewish Feminist.New York: hocken Books.-
Mohamed.S.A. (1990). Kivuli Kinaishi. Nairobi. Oxford
University Press.
Mtembei A.K., (2012). Korasi katika Fasihi: Nadharia Mpya ya
Uhakiki. Chuo Kikuu cha Dar es Salaam: Taasisi ya Taaluma za Kiswahili.
Muhando. P. (1982). Nguzo Mama, Dar es Salaam University
Press, University of Dar es salaam, Tanzania
Njogu,
K & Wafula, R. M. (2007). Nadharia za Uhakiki wa Fasihi. Nairobi.
Jomo Kenyatta Foundation Collage
Njogu,
K. & Chimera, R. (1999). Ufundishaji wa Fasihi. Nairobi. Jomo
Kenyatta
Philip
L. Kilbride (1994). Plural Marriage for Our Times Westport Conn.: Bergin &
Garvey.
Ntarangwi, M. (2004): Uhakiki wa kazi za fasihi.
Rock Islands.Augustine college.
Routlendge, (1974). Women in Stuart England and America; The Law of the Father. London: Gage, op. cit.
Shafi, A.S. (1999). Vuta ni Kuvute. Mkuki na Nyota
Publishers, DSM. Tanzania.
Swidler
L. M. E. (1973). The Jewish Marriage
Contract. New York: Arno Press op. cit.
The Toronto Star (1995). Muhammad al Ghazali, Qadaya al Mar`aa bin al
Taqaleed al Rakida wal Wafida. Cairo: Dar al Shrooq, 4th edition Sabiq, op.
cit.
David W. A., (1896). The Jewish Law of Divorce According to Bible and Talmud Philadelphia:
Edward Stern & Con., Inc Publishing Ltd. .,
TUKI (2004). Kamusi ya Kiswahili Sanifu. Nairobi.Oxford University Press
Wamitila, K.W. (2003). Kamusi ya Fasihi. Istilahi na
Nadharia.Nairobi.Focus
Wamitila, K. M. (2002). Uhakiki wa Fasihi, Misingi na Vipengele vyake. Nairobi: Phoenix.
No comments:
Post a Comment
syliverymanyama@gmail.com