Flower
Flower

Thursday, February 6, 2020

Michakato ya kifonolojia katika uundaji wa maneno kwa kutumia data

Data, kwa mujibu wakamusi ya isimu na falsafa (2004;25) imefasili data kuwa ni jumla ya habari au taarifa zilizokusanywa kwa ajili ya kufanyia uchunguziwa kipengele au vipengele maalum vya kiisimu. Pia umbo la ndani kwa mujibu wa massamba na wenzake (2004:55) wanasema umbo la ndani ni jinsi neno lenyewe lilivyoundwa  na mofimu zake mbalimbali. Michakato, massamba (2004:50 katika isimu ya falsafa ya lugha, ni utaratibu ambao husababisha mabadiliko au mageuko ya kitu kutoka umbo moja na kuingia umbo jingine. Na michakato ya kifonolojia ni hali ya mabasdiliko ijitokezayo inapokuwa vitamkwa viwili hama vimekalibiana, vimegusana au vimeathiriana. Massamba anasema ni utaratibu ambao hauna budi kufuatwa katika uchambuzi na uchanganuzi wa lugha katika ngazi yoyote inayohusika, utaratibu ambao ukifuatwa katika utokeaji wa mabadiliko au sula fulani ya jambo hilo.

Kwa ujumla mtaalamu aliyegundua umbo la ndani na la nje ni Naom Chomsky, pia uhusisha michakato na kanuni za kifonolojia kama vile, udondoshaji, uchopekaji, ukakaishaji, usilimisho pamwe wa nazali na muungano wa irabu.
Kutokana na data (a) mgongo, (b) wezi, (c) woga, (d) chao, (e) salamu, (f) mvua, na (g) mvuvi. Yafuatayo ni maumbo ndani na maumbo nje,
 Umbo la nje                      umbo la ndani
(a)               Mgongo             mu+gongo
(b)               Wezi                 / wa+izi/
(c)               Woga                / u+oga/
(d)               Chao                 / ki+ao/
(e)               Salamu              / salam/
(f)                Mvua                 /n+vua/
(g)               Mvivu                /n+vivu/
Kutokana na kuangalia maumbo ya ndani zifuatazo nui kanuni na michakato iliyojitokeza katika data ihi,
Data (a) mgongo, umbo lake la ndani ni /mu+gongo/ na mchakato wake uliojitokeza ni udondoshaji, kwa mujibu wa Massamba na wenzake (2004:55) anasema kanuni hii inahusu kuachwa kwa sauti fulani katika matamshi wakati mofimu mbili zinapokubaliana yaani katika mazingira hayo sauti ambayo hapo awali ilikuwepo hutoweka. Pia kwa mujibu wa Mugullu (1999:90) anasema irabu hudondoshwa zaidi pale ambapo irabu mbili au zaidi zinazofanana huwa zimefuatana, tuseme penye shadda kla irabu kuliko mahali pengine ambapo hapana shadda lolote la irabu. Kwa ujumla udondoshaji ni moja kati ya michakato isiyo ya kisilimisho ambapo sauti hudondoshwa inapokabiliwa na mazingira fulani ya kifonetiki.
Kutokana na fasili hizo na data, kanuni iliyojitokeza katika mchakato wa udondoshaji katika data hii ni kama ifuatavyo, /u/ [Ө ]/m k, irabu /u/ imebadilika na kuwa kapa katika mazingira ya kutanguliwa na nazali [m] na kufuatiwa na konsonati halisi.
Data (b) wezi, umbo lake la ndani ni /wa+izi/ na mchakato uliojitokeza ni muungano wa irabu. Muungano wa irabu kwa mujibu wa Massamba na wenzake (2004:59) anasema ni uwezekano wa irabu ya mofimu moja kukabiliana na irabu ya mofimu nyingine kisha irabu hizo mbili zikaungana na kuzaa irabu moja tu. Kwa ujumla muungano wa irabu ni mchakato unayohusu uunganishaji wa irabu mbili kuzalisha irabu nyingine mpya, hivyo kanuini ya mchakato huu ni, /a/+/i/→ [ԑ]. Irabu /a/ na irabu /i/ zimekubaliana na kuzalisha irabu mpya ambayo ni [ԑ].
Data (c) woga, umbo lake la ndani ni /u+woga/ na mchakato uliojitokeza ni uyeyushaji. Uyeyushaji ni badiliko la irabu kuwa kiyeyusho, katika kiswahili irabu za juu /i/ na /u/ zikifuatana na irabu isiyofanana nayo katika neno hubadilika na kuwa kiyeyusho, irabu /u/ hubadilika na kuwa kiyeyusho [w], na irabu /i/ hubadilika na kuwa kiyeyusho [j]. Hivyo kutokana na data hii kanini yake inakuwa kama ifuatavyo, /u/→[w]/――I≠u. Sauti /u/ inabadilika kuwa [w] katika mazingira ya kufuatiwa na irabu isiyofanana na irabu /u/.
Data (d) chao, umbo lake la ndani ni /ki+ao/ mchakato wake uliojitokeza ni ukakaishaji, kwa mujibu wa Mgullu (1999:87) akimnukuu Lass(1984) anaeleza kuwa ukakaishaji wa fonimu hutokea wakati ambapo fonimu zisizo za kaa kaa gumu zinapobadilika na kuwa fonimu za kaa kaa gumu. Katika lugha ya kiswahili fonimu za kaa kaa gumu ni mbili tu yaani /ɟ/ / na /ʦ/. Kanuni yake ni, /k/→[tʃ]/―/i/+I≠/i/. Sauti /k/ hubadilika na kuwa [tʃ] katika mazingura ya kufuatiwa na irabu /i/ na irabu isiyofanananayo.
Data (e) salamu, umbo lake la ndani ni /salam/. Mchakato uliojitokeza katika data hii ni uchopekaji, mchakato huu huusisha kuongeza sauti mahali ambapo haikuwepo. Katika kiswahili mchakato huu si dhahiri sana japo hutokea katika maneno ambayo yamekopwa toka lugha nyingine na kuongezwa sauti wakati wa usanifishaji wake. Kanuni inayojitokeza katika data hii ni, [Ө]→/I/ /k―≠, sauti kapa [Ө] inabadilika na kuwa irabu katika mazingira ya kufuatiwa na konsonati halisi.
Data (f) mvua na (g) mvivu, ambapo maumbo yake ya ndani ni /n+vua/ na /n+vivu/, mchakato unaojitokeza katika data hizi mbili ni usilimisho pamwe wa nadhali. Kwa mujibu wa Mgullu (1999:92) anasema tuite fonimu jumuishi /N/ ambayo hujidhihirisha kwa sura  kwa sura mbalimbali za nazali kutegemea na usilimisho ambao fonimu jumuishi hiyo hupata. Pia kwa mujibu wa Besha (1994:45) anasema usilimisho huu ni mnyumbuo unaohusu kuathiriwa kwa sauti zinazofuatana, lakini kwa sharti kwamba sauti hizo ni sehemu za vipashio tofauti vya kisarufi. Kwa ujuusilimisho pamwe wa nazali ni ile hali ambayo nazali  hufuata mahali pa matamshi pa konsonati inayofuatia. Hivyo kutokana na data (g) mvivu yenye umbo la ndani /n+vivu/ kanuni ya hujitokezaji wake ni, /n/[ ]//v/. Nazali /n/ inabadilika na kuwa [ ᶬ] katika mazingira ya kufuatiwa na konsonati halisi /v/. Pia katika data (f) mvua, yenye umbo lake la ndani ni /n+vua/ kanuni ya hujitokezaji wake ni /n/→[ᶬ]/―/v/. Hivyo nazali /n/ imebadilika na kuwa [ᶬ]  katika mazingira ya kufuatiwa na konsonati halisi.
Kwa ujumla kanuni na michakato hii ya kifonolojia imekuwa na umuhimu mkubwa katika uundaji wa maneno ya lugha malimbali pia kwa kuzingatia kanuni na michakato hiyo katika maneno ya lugha ya kiswahili pia kuna vighairi vyake kwani kuna baadhi ya maneno ambayo hughairi kanuni hizo.
                                     
                                                               MAREJEREO
Besha, R.M. (1984). Utangulizi wa lugha na isimu. Dar es salaam. Macmillan Aidan ltd.
Habwe, J na Karanja P (2004) Misingi ya sarufi ya kiswahili. Phoinex publisher. Nairobi
Lass, R.(1984). Phonology. Cambridge university press. Cambridge
Massamba, P. B (2012) Misingi ya fonolojia. TATAKI. Dar es salaam.
Mgullu, R. S (1999) Mtaala wa isimu, fonetiki na fonolojia ya lugha ya kiwsahili.                              
                  Longman  publisher. Nairobi.
TUKI (1990) Kamusi sanifu ya isimu ya lugha. Chuo kikuu cha Dar es salaam.





                     

No comments:

Post a Comment

syliverymanyama@gmail.com

AddToAny